Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Spika, pongezi kwa Wizara hii kwa kazi nzuri wanayoifanya kwa kuboresha mfumo wa habari Tanzania, pamoja na mambo mazuri yanayofanyika lakini nipende kutoa ushauri kwa yafuatayo:-

(1) Kuboresha zaidi televisheni ya TBC kwa mfano mitambo ya radio;

(2) TBC kusikika Tanzania nzima

(3) Maslahi ya wafanyakazi; na

(4) Mafunzo kwa wafanyakazi yawepo. Mheshimiwa Spika, kuhusu michezo nashauri:-
(1) Kuboresha viwanja vya michezo katika Wilaya na Mikoa;

(2) Kukuza michezo kwa vyuo, sekondari na shule za msingi;

(3) Vijijini kuna vijana wanaoweza kucheza mipira, riadha na michezo mbalimbali, lakini wanakosa msaada wa vifaa na viwanja vya michezo; na

(4) Viongozi ni tatizo kubwa wapo kwa ajili ya maslahi siyo kukuza vipaji vya michezo.

Mheshimiwa Spika, mwisho naomba mchezo wa ngumi na riadha itiliwe mkazo ili waliletee Taifa sifa.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.