Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hongera na utekelezaji wa majukumu ya Wizara. Ili kuwasaidia Watanzania walio wengi wanaosumbuliwa na magonjwa makubwa, mfano magonjwa ya moyo, ni vema Serikali iwekeze sana kwenye Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete inayoshughulika na magonjwa ya moyo. Vifaa vyote vinavyotakiwa kwa ajili ya matibabu ya moyo vinunuliwe kwani kuwa na Madaktari Bingwa peke yake bila vitendea kazi haitasaidia. Kwa kuboresha Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Serikali itaokoa fedha nyingi sana ambazo zingetumika kuwatibu wagonjwa wetu nje ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.