Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Dr. Haji Hussein Mponda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. Napenda kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na Watendaji wote wa Wizara kwa kutekeleza majukumu yao vizuri pamoja na changamoto mbalimbali zinazoikabili Wizara na Serikali kwa ujumla. Hakika mimi binafsi naridhika sana na utendaji wao na nawaomba waendeleze ubunifu, uadilifu na kujituma katika kuwahudumia Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu nitauelekeza zaidi kwenye changamoto ya uhaba wa vituo vya tiba katika Wilaya ya Malinyi (Morogoro). Wilaya ya Malinyi ina Kituo kimoja tu cha Afya cha Mtimbira na haina Hospitali ya Wilaya. Halmashauri imependekeza kukipandisha hadhi Kituo cha Afya cha Mtimbira ili kiwe na hadhi kama ya hospitali ili kiweza kuhudumia wananchi wengi wanaohudumiwa na kituo hicho lakini majibu ya Serikali bado hayakubaliani na ombi hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na changamoto za Kituo hicho cha Afya cha Mtimbira, tunaiomba Wizara kuona namna mbadala au kutoa upendeleo wa kipekee kwa kuongeza mgao wa dawa, watumishi, vitendanishi na kadhalika ili kukidhi mahitaji halisi ya wagonjwa wanaohudumiwa na kituo hicho cha afya. Halmashauri kwa kushirikiana na TAMISEMI, tutajitahidi kujenga vituo vingine vya afya katika Halmashauri ya Malinyi lakini katika kipindi hiki cha mpito, tunaiomba Wizara ya Afya kuliangalia ombi letu la Kituo cha Mtimbira kupata hadhi ya hospitali. Ahsante.