Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Suzana Chogisasi Mgonukulima

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. SUZANA C. MGONUKULIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu taarifa ya utekelezaji wa bajeti kwa Fungu 52 inaonesha kuwa hadi mwezi Machi, 2017 Wizara ilikuwa imepokea sh. 314,673,230.000.95 sawa na asilimia 43 ya bajeti ya Wizara, zikiwa ni fedha za matumizi ya kawaida pamoja na miradi ya maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, kuhusu fedha za maendeleo, randama zinaonesha kuwa hadi mwezi Machi, 2017 ni asilimia 34 tu ya fedha za ndani ndizo zilizotolewa na Hazina na kwa fedha za nje ni asilimia sita tu ya fedha hizo zilikuwa zimetolewa na Hazina kwa kipindi hicho. Hii ina maana kwamba bajeti ya maendeleo kwa fedha za ndani haijatekelezwa kwa asilimia 63 na kwa fedha za nje haijatekelezwa kwa asilimia 94. Kwa utekelezwaji huu duni wa bajeti ya maendeleo katika fungu hili, maoni yangu ni kwamba Serikali iwe makini kabisa na afya za Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Fungu 53, kwa mwaka wa fedha 2016 - 2017 Bunge liliidhinisha jumla ya shilingi bilioni
49.9. Kati ya fedha hizo, matumizi ya kawaida ilikuwa shilingi bilioni 41 na shilingi bilioni 8.848 zikiwa ni fedha za maendeleo. Hata hivyo, fedha za maendeleo hadi kufikia Machi, 2017 ni sh. 497,718,250/= sawa na asilimia 5.62 tu ya shilingi bilioni 8.8 zilizoidhinishwa na Bunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii maana yake ni kwamba bajeti ya maendeleo katika fungu hili la Maendeleo ya Jamii haikutekelezwa takriban kwa asilimia 95. Fungu hili ndilo linalohusika na Vyuo vya Maendeleo ya Jamii; na kwa maana hiyo, utekelezaji duni wa bajeti wa vyuo hivyo haviwezi kuwa na uwezo wa kujiendesha na kuzalisha wataalam wa kusaidia jamii zetu kujiletea maendeleo kwa kuweza kuibua fursa zilizo katika jamii zao.