Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Gibson Blasius Meiseyeki

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arumeru-Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. GIBSON B. MEISEYEKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri wa Afya pamoja na Naibu wake kwa kazi nzuri. Pamoja na pongezi hizo, kwa kifupi, lazima niwaombe mambo mawili, matatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Ambulance mbili kwa Halmashauri ya Arusha DC kwa ajili ya Kata zangu mbili za Oldonyowas na Kata ya Bwawani. Hali za wanawake na watoto kwa maeneo haya ni mbaya. Panapotokea dharura, wanataabika sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali yetu ya Mkoa haina mashine za X-Ray, CT-Scan na MRI na hata huduma ya Utra sound haitolewi hospitalini hapo. Umuhimu wa vifaa hivi katika


hospitali kama Mount Meru, wote tunaujua. Mheshimiwa Waziri atusaidie wakazi wa Arusha na viunga vyake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba huduma za Bima za NHIF na CHF ziboreshwe ili wananchi wawe na imani nayo, ili waweze kujiunga kwa wingi na mifuko hii iweze kuwa na tija na iweze kupata uwezo zaidi. Kwa sasa hata sisi wanasiasa tunaogopa kuwahimiza wananchi kujiunga na mifuko hii, kwani changamoto za matibabu ni nyingi mno.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni haya tu kwa sasa.
Shukrani.