Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, tafiti zinaonesha kuwa ugharamiaji mdogo umedhoofisha miundombinu ya utoaji wa huduma za afya nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, takwimu za BRN mwaka 2014 zinaonesha kuwa matumizi ya Serikali katika Afya ni asilimia 11.1 ya matumizi yote ya Serikali. Sekta hii ni muhimu kwa ustawi wa jamii yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zahanati nyingi katika Halmashauri zote za Katavi, Nsimbo, Mlele na Mpanda; asilimia 90 ya zahanati hizi za Katavi ziko nje ya mji. Kwa jiografia, ni ngumu kidogo. Wananchi wanateseka, wanasafiri kutoka Kata ya Kabage Jimbo la Tanganyika, umbali wa kilometa zaidi ya 40 kufuata zahanati katika Kata ya Isengule au Kapala, Msenga, anafika Zahanati ambayo haina dawa wala Wauguzi. Nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kila kata inapata huduma za afya bila kusafiri umbali mrefu kiasi hiki? Huu ni unyanyasaji kwa watu wa vijijini hususan Katani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka huu wa Fedha Serikali ilitenga shilingi 1.99 sawa na asilimia 9.2% ya bajeti yote ya Serikali. Bajeti ni ndogo sekta hii ni kubwa mno na Wizara ni pana, naomba iongezewe bajeti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili tuwe na jamii yenye uwezo kwa kuchangia katika ujenzi wa uchumi, hatuwezi kukwepa kuwekeza ipasavyo kwenye Sekta ya Afya. Ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Hospitali ya Mkoa Katavi? Hospitali iliyopo ni ndogo na mahitaji ni makubwa mno. Oxygen Machine ni moja tu haikidhi mahitaji ya Wanakatavi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2016 alifariki Mkurugenzi wa Manispaa ya Mpanda. Inawezekana tungekuwa na mashine za oxygen mbili au tatu, Mkurugenzi angepona kwa sababu siku hiyo Mkurugenzi huyu anapata shida ya kupumua, mashine ilikuwa inatumiwa na mama mjamzito aliyekuwa hoi threatre. Je, hamwoni kwamba kwa uchache huu Serikali itaendelea kupoteza watu na viongozi bila sababu zisizo na msingi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba Wizara iangalie Mkoa wa Katavi, iongeze bajeti, vifaa tiba, dawa na BP machine.