Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

HE. QULWI W. QAMBALO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Karatu ina umri wa zaidi ya miaka 20 na bado haina Hospitali ya Wilaya. Wananchi wengi na hasa wazee, akinamama na watoto wanapata shida sana kufuata matibabu mbali. Tunacho Kituo cha Afya Karatu ambacho kina miundombinu ya kutosha na kama Wilaya na Mkoa tumekubaliana kupandishwa hadhi kuwa Hospitali ya Wilaya.

Namwomba Mheshimiwa Waziri wa Afya aone umuhimu wa kupandisha hadhi kituo hicho ili kichukue nafasi ya Hospitali ya Wilaya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunayo sera katika Wizara hii inayosema kuwa na dispensary kila kijiji na Kituo cha Afya kila Kata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Karatu ina Kata 14 na ni Kata tatu tu zenye Vituo vya Afya. Huu ni upungufu mkubwa sana. Hata hivyo, vitatu vina upungufu mkubwa wa vifaa tiba na watumishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ziko dispensary zimefungwa kwa kukosa watumishi mfano Zahanati ya Makhomba Endashangwet na kadhalika. Suala la afya ya wananchi wetu ni suala muhimu sana. Nchi yetu ni ya wakulima na ili mtu alime anahitaji afya timamu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la maendeleo ya Jamii limesahaulika kabisa. Kitengo hiki kinapaswa kuwa injini katika Halmashauri zetu maana hawa ndio wanapaswa kufanya maandalizi ya jamii ili mradi iweze kufanikiwa. Huko nyuma tulikuwa na Vyuo vya Maendeleo ya Jamii, mfano Tengeru, Monduli na kadhalika. Vyuo hivi vimetoa wataalam wazuri sana wa kuwahamasisha wananchi kupokea miradi na kuwaandaa ili mradi iwe endelevu. Hali ilivyo sasa, kitengo hiki kimemezwa na Idara ya Afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali iwawezeshe watumishi wa Sekta ya Maendeleo ya Jamii ili wawafunze wananchi kwa utekelezaji wa miradi.