Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote napenda kumpongeza Waziri, Mheshimiwa Ummy Mwalimu kwa kazi kubwa anayoifanya katika kuiongoza Wizara hii. Pia nampongeza Mheshimiwa Dkt. Kigwangalla kwa jinsi ambavyo anamsaidia Waziri wake na kujibu maswali kwa ufasaha kabisa Bungeni. Pia nichukue nafasi hii kuipongeza timu yote ya Wizara ya Afya chini ya Katibu Mkuu kwa jitihada zinazoendelea kufanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuwashukuru kwa kushirikiana na TAMISEMI na Wilaya yangu kuwa katika Mpango wa Kuboresha Vituo vya Afya, hususani Kituo cha Afya cha Mkili. Hata hivyo, kuna Kituo cha Afya cha Kihagara ambacho kinaendelea na ujenzi. Nitaomba tupewe jengo moja tu kwa mwaka huu kwa ajili ya wodi ya wanawake kwa kuanzia na upande mwingine wanaweza wakakaa watoto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Nyasa, with a very beautiful land kwa sasa tuna mpango mkubwa wa Nyasa Maridadi, Nyasa iwe safi, Nyasa ipendeze na hivyo kuwa ni mahali pazuri pa kuishi na kutalii. Idadi ya watu wanaotembelea Nyasa imeongezeka sana. Kitu cha kusikitisha ni kuwa hakuna uhakika wa usalama wa wananchi hao na watalii kiafya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya hii haina Hospitali ya Wilaya, tunategemea Kituo cha Afya cha Mbamba Bay ambacho hakina Ultra-sound wala X-ray na kadhalika. Tukipata majeruhi lazima wapelekwe Wilaya ya Mbinga au Peramiho na pengine Hospitali ya Rufaa Songea. Hao wananchi wengi wao ni maskini lakini ili kupata vipimo hivi vikubwa lazima walipe gharama ya nauli na baadaye walipe gharama nyingine zaidi kwa ajili ya kujikimu na dawa. Kwa summary naomba mtusaidie Ultra-sound machine, X-ray machine na ambulance, tafadhali sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimboni kwangu kuna malalamiko makubwa juu ya mikopo ya pikipiki iliyotolewa na Benki ya Wanawake wakati Mbunge wa Jimbo akiwa ni Mheshimiwa Marehemu John Komba. Wanadai kuwa wamekuwa wakichangia lakini kila wakati wanatajiwa deni kubwa zaidi. Vile vile ni kuwa ukusanyaji wa madeni hayo hauleweki na wanapokea simu kutoka kwa watu ambao wanakuwa hawana uhakika nao na kuwatishia kuuza mali zao. Ni vema ufanyike mkutano wa wadeni na ikiwezekana nikaribishwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, natanguliza shukrani.