Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naunga mkono hoja hii ya Wizara husika. Naipongeza Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Jemedari Mtukufu Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli na wasaidizi wake wote. Kubwa la msingi tuwaombee mema kwa Mungu. Hata hivyo nina haya machache ya kutaka ufafanuzi na ushauri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inasomesha Madaktari wengi kwa gharama kubwa sana: Je, ina mkakati gani wa kuwa-retain angalau kuwa na mkataba wa win win situation kwani kuna uhaba sana wa Madaktari kutokana na wengine kukimbilia nchi za nje for green pastures? Uzalendo kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, afya ya mama na mtoto inaelekea mwaka huu vifo vimeongezeka. Kutokana na data ambazo zinaeleweka, nini chanzo na mkakati wa kuboresha? Tukumbuke mama ndiye familia. Elimu kwa umma iongezwe kuhusu umuhimu wa kujifungulia hospitali au zahanati. Pia akinamama wengi hawana uwezo, hivyo ni muhimu pia kuwapatia tools za wakati wa kujifungua endapo kutakuwa na dharura.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali ya Rufaa ya Mbeya ina-extend wodi ya watoto kwa juhudi binafsi na ubunifu. Nampongeza sana Mkurugenzi wa Hospitali hiyo Dkt. Mbwanji. Hata hivyo, nahitaji kujua contribution ya Serikali katika ujenzi huo, kwani Hospitali hii ndiyo inayotoa huduma kwa Mikoa yote ya Nyanda za Juu Kusini na kwingineko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimba na ndoa za utotoni ni tatizo sugu nchini kwetu, kwani licha ya kuwakatisha masomo watoto wa kike, pia inawaathiri kiafya na kisaikolojia. Hili suala kwa kiwango kikubwa linatokana na mila potofu na imani nyingine za dini ambapo sasa Serikali ichukue hatua na jitihada za ziada kwa kuzidi kutoa elimu kwa umma, kukutana na wadau husika, mfano makundi ya dini, Machifu na Serikali. Kwa Wizara husika, Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kushirikiana na Wizara ya Katiba na Sheria ilete Muswada wa kubadilisha Sheria hii ya Ndoa na Mimba za Utotoni. Nashauri umri uongezwe toka miaka 14 iwe 18 na hatua kali zichukuliwe kwa wahusika wote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nahitaji kujua why TACAIDS (PM‘s Office); at the same time, why NACP (Ofisi ya Wizara ya Afya office)? Maana wote wanashughulikia masuala ya UKIMWI; huu ni mwingiliano/mgongano wa majukumu na kupoteza fedha za walipa kodi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Azimio la Abuja la asilimia 15 limeshakamilishwa kwa hapa nchini kwetu? MDG’s/SDG’s limefanikiwaje kuhusu yale malengo yake hapa nchini kwetu? Mpango wa Afya ya Msingi (MAM) tunahitaji tupewe data; Serikali imefikia wapi? Kwani hii iko katika Ilani yetu ya Uchaguzi wa CCM na huduma bure.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.