Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Ally Seif Ungando

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia Wizara hii ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Wazee na Watoto. Nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais wetu mpendwa, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi anayoifanya kwa Taifa hili. Pili, nampongeza Mheshimiwa Ummy Mwalimu na Naibu wake, Mheshimiwa Dkt. Hamisi Kigwangalla kwa kazi nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo langu la Kibiti hakuna budi kuishukuru Serikali yetu sikivu kupitia Wizara yake ya Afya kwa kutupatia gari la kubebea wagonjwa (Ambulance) aina ya Toyota Land Curiser kwa ajili ya Kituo cha Afya cha Kibiti. Hii itatusaidia kwa kiasi kikubwa kuzuia vifo vitokanavyo na uzazi na pili, kupata vitanda 20 vya kulazia wagonjwa na vitanda vitano vya kujifungulia na magodoro pamoja na shuka zake. Sisi Wanakibiti kwa ujumla tunamwahidi tutavitunza vifaa hivi vyote pamoja na gari la wagonjwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kila penye mafanikio hapakosi changamoto. Changamoto kubwa ni Ikama ya Watumishi katika Wilaya yangu ya Kibiti. Pia tuna upungufu mkubwa wa watumishi. Vile vile posho zao za masaa ya ziada ya kufanya kazi, madai ya fedha za likizo na motisha kwa watumishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Kibiti hadi sasa haina Hospitali ya Wilaya. Kwa hiyo, inafanya Kituo cha Afya Kibiti kupokea wateja wengi kuliko uwezo wake. Kwa hiyo, tunaiomba Wizara yako itupandishie kituo hiki kiwe Hospitali ya Wilaya. Katika kituo hiki hatuna Mochwari ya kuhifadhia maiti. Pia hakuna ukarabati wa kituo hiki kwa ujumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo langu la Kibiti kuna Kata tano, zipo maeneo ya Delta. Naomba Mheshimiwa Waziri atuangalie kwa jicho la huruma sana, kwani maeneo haya mtu akipata matatizo hakuna msaada wowote. Naomba tupatiwe ujenzi wa theatre ya upasuaji katika Kituo cha Afya Mbwera na kutupatia watumishi wa kutosha Ikama 149; waliopo ni tisa na pungufu ni 140. Naomba tusaidiwe. Kata hizo ni Maporini, Mbuchi, Msala, Kiongoroni na Salale.