Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kutoa pongezi kwa kazi nzuri inayofanywa na Mheshimiwa Waziri wa Afya na Naibu Waziri kwa kazi nzuri wanazofanya. Naishukuru sana Wizara kwa kutupatia gari la Ambulance kwa Kituo cha Lalago na Malampaka. Nashukuru sana kwa uzalendo wa hali ya juu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo kubwa ninalotaka kuchangia ni kuhusu suala la waathirika wa madawa ya kulevya. Kama tujuavyo, kuna madhara makubwa ya kiafya kwa waathirika wa madawa ya kulevya (waraibu). Wizara ina jukumu la kupambana kuzuia baadhi ya madhara hayo ikiwemo maambukizi ya UKIMWI, homa ya ini (hepalitis B), TB na kadhalika. Moja ya shughuli ya kupunguza madhara haya ni pamoja na hatua za Serikali kupitia Sober House, lakini Wizara ina jukumu la kusambaza dawa ya Methodone na Syringe kwa waathirika (waraibu). Tatizo, Wizara haifanyi hivyo. Kuna upungufu mkubwa sana wa Methodone na Syringe. Syringe zinagawanywa na Wilaya moja tu; na Wilaya hiyo ni Temeke tu, Wilaya nyingine hakuna mgawo wa Syringe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri, haioneshi juhudi maalum kwa waathirika hawa. Matokeo yake kundi hili linaathirika zaidi na wengine wanarudi kwenye utumiaji wa madawa hayo na wanapoteza maisha kwa magonjwa mengine nyemelezi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru, naunga mkono hoja.