Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali ya Wilaya ya Ulanga ina hali mbaya sana. Watumishi ni wachache sana kiasi cha kukwamisha matibabu, mfano Madaktari ni wachache, wahudumu pia hakuna, wala mtaalam wa X-Ray machine; wodi ni chache, ndogo na zilizochakaa. Hii inapelekea wagonjwa kuchanganywa ambapo ni hatari; chumba cha upasuaji hakipo katika standard, hakina monitor; Madaktari wanatumia uzoefu tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mashuka na nguo za wagonjwa zinafuliwa kwa mkono (hakuna mashine ya kufulia). Hii ni hatari kwa afya za wafanyakazi. Pia gari la wagonjwa lipo moja ambalo nilinunua mimi Mbunge. Kutokana na jiografia ya Jimbo ilitakiwa kuwa na magari angalau matatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile Wahudumu wa Afya wanajinunulia uniform mwaka wa saba huu (hakuna uniform allowance); kuna upungufu mkubwa wa dawa hasa za ugonjwa wa kifafa, ukizingatia Wilaya ya Ulanga ina wagonjwa wengi sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho ni marupurupu ya wahudumu.