Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, uhaba wa watumishi katika hospitali zetu nchini suala hili limekuwa ni tatizo kubwa sana katika Wilaya zetu. Kwa mfano, Wilaya ya Kalambo, Nkasi, Sumbawanga Mjini na Sumbawanga Vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu saratani ya shingo ya kizazi, suala hili limekuwa ni tatizo kubwa kwa wanawake wa Kitanzania na kasi yake ni kubwa sana, lakini bado hatujaona Serikali ikiipa kipaumbele kulingana na tunavyopoteza wanawake wengi hasa walioko vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la ukosefu wa dawa kwenye hospitali zetu, hili limekuwa ni tatizo kubwa, Serikali ifanye utaratibu wa kufuatalia kama dawa zipo katika hospitali za vijijini. Wizara ipeleke dawa ili kuokoa maisha ya Watanzania wenzetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Sheria ya Ndoa, kuna sababu ya kuleta mabadiliko ya Sheria ya Ndoa ili kuokoa maisha ya watoto wetu wa kike kwa kukosa mambo ya msingi ikiwemo elimu, kwani wakiingia kwenye ndoa wakiwa na miaka 18 itapelekea kukosa elimu.

Kuhusu ukatili kwa wanawake, kwa kuwa ukatili huu umekuwa ukiendelea kwa kasi hasa kwa watoto wa kike wakiwa shuleni, mitaani na nyumbani, je, Serikali inaleta mkakati gani wa kumaliza tatizo hili la ukatili?

Mheshimiwa Mwenyekiti, vifo vya wanawake wajawazito hakuna mkakati wa dhati wa kumaliza tatizo hili na kuona wanawake hasa waliopo pembezoni na wanawake wa vijijini, Serikali iweke kipaumbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la uzazi wa mpango, kuna kila sababu ya Serikali kutoa semina elekezi hasa kwa maeneo ambayo bado elimu hii haijawakomboa kwani kumekuwa na upotoshaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali kwa kupitia Wizara ya TAMISEMI na Wizara ya Afya ili kuboresha na kujenga vituo vya afya kwa kila kata na hospitali za Wilaya hasa katika Mkoa wa Rukwa hakuna Hospitali za Wilaya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kuzingatia, kukosekana kwa hospitali hata moja ya Wilaya katika Mkoa wa Rukwa kunapelekea mlundikano wa wagonjwa kwenye Hospitali ya Mkoa ya Rufaa.