Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Mahmoud Hassan Mgimwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. MAHMOUD H. MGIMWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue fursa hii kuwapongeza sana kwa kazi nzuri Mheshimiwa Waziri pamoja Naibu Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu utajieleza kama ifuatavyo:-

Kuhusu uzinduzi wa zahanati, wananchi wamefanyakazi nzuri za kujenga zahanati, tatizo kubwa lililopo ni uzinduzi wa zahanati hizo kwa sababu ya kukosa wataalam, vifaa pamoja na allocation ya dawa. Naomba sana Mheshimiwa Waziri au Naibu Waziri wa Afya aje kwenye Majimbo yetu ili uzinduzi wa hizo zahanati ufanyike haraka iwezakanavyo ili kutovunja nguvu za wananchi waliojitolea katika ujenzi huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la pili ni vituo vya afya, katika ilani ya chama chetu, tuliahidi kujenga kituo cha afya katika kila kata, naomba sana Serikali ituunge mkono kwenye maeneo haya ya kujenga vituo vya afya hii itakuwa suluhisho la kudumu na kwa namna ya kipekee niipongeze Serikali kwa kujenga vituo vya afya vya mfano kila Jimbo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ni eneo la dawa katika zahanati zetu. Vituo vya afya pamoja na hospitali zetu naomba sana muongeze migao ili wananchi wasiendelee kusumbuka.

Kuhusu tiba kwa wazee ni vema sasa Serikali ikaweka mkakati wa kuhakikisha huduma zote muhimu zinapitika kwa wakati katika kitengo hicho cha wazee na kuwa wanapata dawa kwa wakati na madaktari wawepo wakati wote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja, chapeni kazi.