Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa fursa hii. Nianze kwa kutoa pongezi kubwa kwa Mheshimiwa Waziri Ummy Mwalimu na Naibu wake Mheshimiwa Dkt. Hamisi Kigwangalla kwa hotuba nzuri yenye kuleta matumaini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali ya Wilaya ya Mafia inakabiliwa na changamoto nyingi, lakini kubwa ni ukosefu wa huduma ya x-ray.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mafia ni kisiwa na kutokana na changamoto ya usafiri hospitali hii wananchi wanapata taabu sana kuwasafirisha kufuata huduma ya x-ray Wilayani Temeke, Dar es Salaam. Mimi binafsi kwa kushirikiana na wahisani mbalimbali nimefanikiwa kupata x-ray mpya na ya kisasa na tayari ipo Mafia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa masikitiko makubwa x- ray imefika Mafia toka mwezi Aprili, 2016 mpaka leo hii bado ipo store, haijafungwa. Mheshimiwa Waziri na Naibu wake pamoja Katibu Mkuu wanafahamu suala hili, ukweli nashindwa kuelewa ni kwa nini hamtaki kutoa ruhusa x-ray ili ifungwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kujenga chumba kipya kwa ajili ya x-ray mpya siyo wazo baya ila ombi letu ni x-ray mpya ifungwe katika chumba cha x-ray ya zamani na ile ya zamani chumba kipya kitakapokuwa tayari ifungwe. Hii itasaidia sana kwani kwa sasa wananchi wanapata usumbufu mkubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hopitali ya Mafia pia haina jokofu la kuhifadhia maiti. Suala hili ni muhimu sana kutokana na kukua kwa sekta ya utalii na shughuli za kijamii kuongezeka, inapotokea dharura ya mtu au watu kufariki ambao siyo wenyeji kwa Mafia usumbufu mkubwa unajitokeza kama ilivyotokea kuanguka ndege ya Comoro.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kuipandisha hadhi zahanati ya Kironywe kuwa kituo cha afya; Mheshimiwa Waziri, Wilaya ya Mafia yenye jumla ya vijiji 23 na kata nane haina kituo cha afya hata kimoja. Tayari hatua za awali tumeshazikamilisha tunaomba Wizara sasa iharakishe mchakato huu ili Wilaya tuwe na kituo kimoja cha afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zahanati za Bwejuu, Mlongo, Gonje na Jimbo zilitengewa fedha ili kumalizia mabomba, lakini mpaka sasa tumekapokea robo tu ya fedha hizo. Kwa namna ya kipekee zahanati ya Bwejuu ambayo ipo katika kisiwa kidogo cha Bwejuu ambapo hakuna huduma yoyote ile ya kitabibu, hakuna hata sanduku la msaada wa kwanza (first aid kit) tunaomba Serikali iharakishe upatikanaji wa fedha hizo ili wananchi wapatoa 1,000 wa kisiwa cha Bwejuu wapate huduma hii muhimu.

Kuhusu Mfuko wa Bima ya Afya tunaomba Serikali iboreshe CHF ili iweze kutumika mpaka ngazi ya Mkoa na pia huduma za upasuaji zijumuishwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba mgao wa vitanda na mashuka kipaumbele tupewe Wilaya za pembezoni kama Mafia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.
Ahsante.