Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Hawa Abdulrahiman Ghasia

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mtwara Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchukua fursa hii kumpongeza Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu Afya na Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii pamoja na wataalam wao kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumshukuru Waziri kwa kukipatia gari kituo cha afya cha Kitere, suala ambalo nina imani litasaidia sana katika kuboresha huduma za rufaa kwa wagonjwa hasa akina mama na watoto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamuomba Mheshimiwa Waziri kuongeza watumishi wa afya katika vituo vya afya vya Nanguruwe, Kitere na Mahurunga ili viweze kutoa huduma bora kwani vituo hivyo vinavyo vifaa vya kisasa vya kutolea tiba, lakini baadhi yake vinashindwa kutumika kutokana na uchache wa wataalam wenye weledi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaiomba Serikali pia kuongeza udahili wa wauguzi, maafisa tabibu, wafamasia na wataalamu wa maabara na kufadhili masomo yao ili tuweze kuwapa masharti ya kwenda kufanya kazi katika maeneo yenye upungufu kwa muda maalum.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niiombe Serikali kuonesha nia ya dhati katika ujenzi wa hospitali ya Kanda ya Kusini. Kwa Kusini Mkoa wa Lindi na Mtwara ni kanda pekee isiyokuwa na Hospitali ya Rufaa ya Kanda na kwa miaka miwili mfululizo kiasi kinachotengwa kwa hospitali hiyo kwanza ni kidogo na pili, fedha hizo hazitolewi. Kwa kifupi ni kama ujenzi umesimama, Mheshimiwa Waziri iwapo hutatoa mikakati inayotia moyo na yenye kuonesha nia ya kukamilisha ujenzi wa hospitali hii nakusudia kuondoa shilingi kwenye mshahara wa Waziri na kwenye bajeti ya Wizara.

Mheshimi Mwenyekiti, naunga mkono hoja.