Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Augustine Vuma Holle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. AUGUSTINO M. MASELE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja ya Mheshimiwa Waziri kwa hotuba nzuri. Afya ni msingi wa maisha ya binadamu awaye yote kwa vile kuwa na afya mgogoro ni chanzo cha kufilisika kwa shughuli zote za maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa bahati mbaya kabisa Wilaya yetu ya Mbogwe mwaka huu wa fedha Halmashauri yetu iliweka katika bajeti yake jumla ya shilingi bilioni 1.5, hata hivyo kutokana na ukomo wa bajeti fedha hizo zikaondolewa kwenye bajeti. Naishauri Serikali yetu ione umuhimu wa kusaidia ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Mbogwe. Tuna taabu Mbogwe, sikieni kilio chetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali kwa kutujengea theatre mbili katika vituo vya afya vya Masumbwe na Mbogwe ambapo Shirika la Umoja wa Mataifa la UNFPA kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na kuvipatia vituo hivi vya afya ambulance mbili, hongereni sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo kituo cha afya cha Mbogwe bado hakijafunguliwa rasmi kwa vile vifaa havijakamilika katika theater licha ya kwamba kweli gari la wagonjwa la UNFPA lipo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mbogwe tuna uhaba mkubwa wa watumishi katika Idara ya Afya kwenye vituo vya afya na zahanati, naiomba Serikali ilione jambo hili na itupatie watumishi wa kutosha Wilayani kwetu.

Mhesimiwa Mwenyekiti, aidha naiomba Serikali itusaidie kukamilisha ujenzi wa vituo vya afya vya Ilolangula Ikunguigazi, Ikobe, Nhomolwa, pamoja na ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Mbogwe ili kuboresha huduma za afya Wilayani Mbogwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Geita ni mpya tunahitaji hospitali ya rufaa yenye uwezo wa kuhudumia wananchi wilayani wanapopata rufaa. Ujenzi wa hospitali ya rufaa utakuwa ukombozi kwa wananchi wa Mkoa mpya wa Geita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hotuba ya Mheshimiwa Waziri.