Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na kumpongeza Waziri Mheshimiwa Ummy Mwalimu, Naibu Waziri Mheshimiwa Kigwangalla na watendaji wote wa Wizara kwa kuwasilisha hotuba yao hapa Bungeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sekta ya afya ni moja ya sekta nyeti Tanzania inayosimamiwa na Wizara ya Afya pamoja na hospitali zote za rufaa, hospitali za wilaya pamoja na vituo vya afya na zahanati zilizopo chini ya Serikali za Mitaa, Manispaa na Wilaya hizi zipo chini ya Wizara ya TAMSEMI, pamoja na kwamba zote zinapatiwa miongozo ya kiutendaji kutoka Wizara ya Afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na umuhimu wa Idara ya Afya katika Mkoa wetu wa Iringa, inakabiliwa na changamoto zifuatazo:-

i) Chumba cha uangalizi wa wagonjwa wa nje wa dharura (OPD) hivyo kusababisha msongamano mkubwa katika wodi kwa zile huduma zinazohitajika uangalizi wa muda mfupi.

(ii) Wastani mdogo wa daktari kwa wagonjwa. Hivyo kufanya kuwa na msongomano mkubwa katika vyumba vya madaktari wachache wanapokuwa zamu, hivyo kuongeza work load kwa madaktari.

(iii) Kuna wodi nzuri za watoto zilizojengwa kwa ufadhili wa Hospitali ya Vicensa ya Italy na mzalendo mmoja familia ya ASAS lakini hakuna Daktari Bingwa wa Watoto (Pediatrician) pamoja na idadi kubwa ya watoto wanaolazwa hospitalini hapo.

(iv) Hakuna kitengo cha ENT (sikio, pua na koo) wala Daktari wa ENT. Hivyo case zote za ENT lazima zipewe rufaa au kusubiri visiting doctor ambayo inakuwa ni kero kwa wagonjwa wenye matatizo yanayohusiana na tatizo hilo.

(v) Vitendea kazi muhimu wodini ni vichache kama vile oxygen cylinder na oxgen concentrators, pulsonetor za kupima kiwango cha oxygen kwa mgonjwa, BP machine hazina uwiano inaostahili kwa ugonjwa (wodi nzima inakuwa na mashine moja tu), vipimo vya sukari kwa wagonjwa wa sukari waliopo wodini wanaohitaji uangalizi wa kina.

(vi) Kitengo cha afya ya akili hakikidhi haja na mahitaji ya wagonjwa wa afya ya akili kwa sababu kina vyumba vinne yaani viwili kwa wanaume na viwili kwa wanawake, vyenye uwezo wa kukaa na wagonjwa wawili kila chumba, hivyo uwezo wa hospitali kuhudumia wagonjwa wa akili ni wagonjwa wanne tu, ambavyo ni hatari kwa hospitali yenye kiwango cha Hospitali ya Mkoa ya Rufaa ukizingatia Mkoa.

(vii) Wagonjwa wanaostahili msamaha hawapati huduma za dawa kama inavyostahili kutokana dawa nyingi kutokuwepo hospitalini, hivyo kusababisha shida zaidi kwa wagonjwa wasio na uwezo, wazee na wenye magonjwa ya kudumu kama sukari, akili, TB na HIV.

(viii) Nyumba za madaktari zaidi ya asilimia 85 ya madaktari na wahudumu wengine wa afya wanakaa maeneo ya mbali na hospitali kutokana na kukosekana nyumba hasa nyakati za usiku kwa wagonjwa wetu.

(ix) Kukosekana kwa huduma zingine za msingi kama CT Scan, MRI, ECG, ECHO katika hospitali ya Mkoa hivyo kusababisha rufaa zingine zisizokuwa na lazima ambapo ni kero kwa wananchi wanaohitaji huduma hizo.

(x) Mifumo ya ki-eletronic inayowezesha daktari kupata majibu ya mgonjwa kutoka maabara na taarifa nyingine za mgonjwa kwa haraka kama ilivyo hospitali nyingine za private.

(xi) Pia dawa muhimu hazipo hospitalini kila wakati, hivyo kusababisha wagonjwa kuhangaika kwenda kutafuta maduka binafsi na kero zaidi inakuwa wakati wa usiku ambapo hayo maduka binafsi yamefungwa, inaweza kuhatarisha maisha ya mgonjwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Benki ya Wanawake; niipongeze Serikali kwa kuweka dirisha la kuweza kuhudumia wananchi wa Mkoa wa Iringa, lakini ili ile dhamira ya kuanzisha benki hii kwa ajili ya wanawake ipate kutimia. Pia kuwepo na mobile agency kwa ajili ya huduma hii kufikishwa vijijini kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la vituo vinavyolea watoto yatima; pamoja na wamiliki wa vituo hivi vya watoto yatima kuisaidia Serikali katika wimbi hili la watoto yatima na watoto wa mtaani, lakini kuna changamoto nyingi zilizopo katika vituo hivi. Kuna vituo havina hata uwezo wa kuwatibu watoto hawa wanapougua au kupata ajali. Hivyo ni vema Serikali ikaweka utaratibu wa kusaidia vituo hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.