Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Ester Michael Mmasi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. ESTER M. MMASI: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi napenda nichukue fursa hii niweze kuchangia mawazo yangu katika Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa mwaka wa fedha 2017/2018. Kabla sijakwenda moja kwa moja kwenye mada zangu naomba kwa heshima na dhati ya moyo wangu nimpongeze Mheshimiwa Ummy Mwalimu kwa juhudi zake mahsusi katika usimamizi na uendeshaji wa masuala ya afya ya Mtanzania, afya ya akina mama na watoto pamoja na afya ya ustawi wa jamii yetu hususani kwa rika la vijana na wazee pia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu afya ya mzazi, Mheshimiwa Waziri pamoja na juhudi zako za dhati katika kunusuru akina mama wanaojifungua lakini pia na watoto wachanga bado tunayo changamoto kubwa sana kwenye vifo vya akina mama wanapojifungua. Takwimu zinaonesha kwenye kila vizazi hai 100,000 tuna vifo 556 vya kina mama wanopoteza maisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niiombe Serikali yangu, sambamba na changamoto hii ya vifo vya akina mama wanaopoteza maisha pindi wanapojifungua lakini tunayo changamoto kubwa ya vifaa tiba na miundombinu ya kitabibu kwa upande wa tiba za watoto wachanga. Ni kweli tuna vifo vingi vya kina mama pindi wanapojifungua lakini pia tuna vifo vingi vya watoto wadogo/wachanga kutokana na changamoto ya uwepo wa PRE NATAL ICU (PI) kwa watoto under five years.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kitendo kinachokatisha tamaa na morale ya matabibu walio wengi nchini Tanzania hususan katika Hospitali ya Muhimbili ambayo kimsingi wamekuwa na historia ya kazi nzuri ya kitabibu ya kuokoa maisha ya vichanga especially pale inapotokea emergence ya upasuaji kwa watoto wachanga. Wengi wa madaktari wamewahi kusema tumekuwa na kazi nzuri theatres lakini kazi zetu nyingi zinaharibikia kwenye vyumba tunapowalaza watoto wagonjwa ambao wamewahikufanyiwa upasuaji kwa kuwa vyumba vya ICU kama PRE NATAL ICU zimekuwa na msongamano mkubwa wa watoto kwa kuwa katika Hospitali za Mikoa, Wilaya na Halmashauri hatuna huduma za vyumba vya watoto za PRE NATAL ICU.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ushauri wangu kwa Serikali yangu kuwa Wizara hii iweze kuongezewa fungu la uboreshaji wa miundombinu ili hospitali zetu ngazi za Mikoa na Wilaya ziweze kupata wodi za PRE NATAL ICU ili kunusuru vifo vya watoto wachanga. Sambamba na hili pia niombe Serikali yangu iangalie kwa jicho la kipekee kabisa vifo vya kina mama wanaopoteza maisha pindi wanapojifungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunayo changamoto kubwa ya afya ya akina mama especially case ya cancer ya shingo ya kizazi. Ni rai yangu kwa Serikali kupitia taasisi za tafiti za afya ya binadamu tuweze kufanya utafiti wa kina ili kubaini nini changamoto tulizonazo kwenye mfumo mzima wa afya ya mama na msichana ambayo inasabisha ongezeko la ugonjwa wa cancer ya shingo ya kizazi. Sanitary towels zote zinazosambazwa kwa umma wa Watanzania zifanyiwe utafiti wa kina, jamii zenye mila za kutotahiri wanaume nazo zifanyiwe tafiti za kina ili kubaini kwa nini ongezeko kubwa la cancer ya kizazi. Ikiwa HPV Vaccine ndiyo jawabu la kinga ya maambukizi basi Serikali yangu ije na majibu kwa umma wa Watanzania ili tupate suluhisho la kudumu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wasichana waliopo kwenye umri mdogo wanapoteza maisha kwa kasi isiyokubalika, tuiombe Wizara itusaidie kuja na suluhisho la kudumu kwenye suala zima la ongezeko la cervical cancer.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu HIV & AIDS, ni kweli tunayo changamoto kubwa ya tiba na vifaa tiba pamoja na mifumo ya uendeshaji tiba kwa watu wenye maambukizi ya VVU. Kupitia data ya USAID Novemba, 2016 Serikali ya Tanzania imekuwa ikichangia kwenye tiba ya HIV & AIDS kwa asilimia tatu tu ikilinganishwa na michango ya nchi wahisani kama mathalani USA ambayo imekuwa ikichangia takribani asilimia 71.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunayo changamoto ya utegemezi mkubwa kwenye dawa za ARV kutokana na kwamba mifumo ya TEHAMA ambapo asilimia 100 ya mifumo ya kitabibu imetengenezwa na kufadhiliwa na Wamarekani. Naona shida kuona hata masuala ya mifumo ya uendeshaji wa tiba ya wagonjwa walioathirika CTC2 (Care & Treatment Clinic) ambayo mfumo huu unatumika katika kuhifadhi kumbukumbu za wagonjwa wote walio na maambukizi ya VVU, DI+IS 2. Mfumo huu nao unatumika kuhifadhi kumbukumbu za wagonjwa; kwa kitaalam mfumo huu unatambulika kama District Health Information System ambao nao unafadhiliwa na Wamarekani kwa asilimia 100.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi napata taabu sana kuona tunashindwa kuendana na principle ethics za namna ya kuhifadhi ama kutunza usiri wa wagonjwa hawa ikiwa mifumo hii itaachiwa mashirika ya nje waitengeneze na kuifadhili. Je, nini nafasi yetu kama nchi katika kulinda privacy za wananchi wetu wenye maambukizi ya VVU? Ni dhahiri kabisa kwa utendaji huu hatuna assurance ya sustainability ya mifumo hii na hata tiba za dawa ikiwa Tanzania itakubali kusimama kama mtizamaji. Three percent of contribution as a country is too peanut for us to stay safe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu kwa Serikali ni kwamba ione sababu za msingi katika kutumia rasilimali ya Tanzania kwa ajili ya kuunda mifumo ya kitabibu. Ndani ya DIT (Dar es Salaam Institute of Technology) tunao vijana wazuri wenye umahiri mkubwa katika kuunda software kama software developers na vijana hawa wana utaalam na uzoefu wa kutosha kwenye masuala ya programming, tuwape nafasi vijana wetu wa Kitanzania kwenye ushiriki mzima wa masuala ya TEHAMA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga hoja mkono juhudi za Serikali kupitia wasilisho la hotuba hii muhimu kwa ustawi mzima na afya ya kina mama na watoto. Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Serikali ya Awamu ya Tano ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.