Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali kwa kazi nzuri inayoendelea. Katika sera ya zahanati kila kijiji/mtaa na kituo cha afya kila kata, pia hospitali ya wilaya na mkoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Singida Mjini kwa asili ya mji ulivyo karibu kata nane za mjini zinategemea Hospitali ya Mkoa. Hivyo ninaiomba Serikali kuharakisha kuanza kazi kwa Hospitali ya Rufaa ili Hospitali ya Mkoa ihamie kwenye Hospitali inayojengwa sasa hivi na eneo/majengo ya Hospitali ya Mkoa yatumike kama Hospitali ya Wilaya, tutakuwa tumemaliza tatizo la Singida Mjini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu damu salama, mpango huu ni mzuri sana na unasaidia sana wananchi hususani Singida Mjini. Changamoto inayojitokeza hapo ni kama ifuatavyo:-

(i) Mwamko mdogo kwa wananchi kuchangia damu;
na
(ii) Halmashauri hazitengi bajeti kwa ajili ya zoezi hilo
hususan Singida Mjini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tangu mwezi Juni, 2016 hadi Februari, 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Singida imekusanya unit 12 tu out of 2300 za mkoa mzima. Hivyo tunaishi kwa kutegemea Wilaya nyingine au tunatumia damu isiyo salama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali ifanye tathmini kwenye jambo hili. Pia Mganga Mkuu wa Mkoa awe na mamlaka ya kuisimamia Halmashauri katika kutekeleza jambo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu fedha za dawa, ninaishukuru sana Serikali kwa kutoa fedha Singida Mjini takribani shilingi 203,100,000 ambayo ni sawa na asilimia 93. Tatizo tunalolipata dawa hazionekani, nakosa majibu ya kuwaambia. Naiomba Serikali itusaidie kusimamia upatikanaji wa dawa.