Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Rombo hatuna Hospitali ya Wilaya. Hata hivyo Kituo cha Afya cha Karume Usseri kinaandaliwa kwa ajili hiyo. Hivi sasa majengo yote muhimu yapo tayari kasoro jengo la OPD ambalo ujenzi wake uko ngazi ya msingi. Ujenzi umesimama kwa sababu ya deni tunalodaiwa na mkandarasi. Tunaiomba Serikali kutusaidia kumalizia deni hilo na kutoa pesa ili kuharakisha ujenzi wa jengo hilo ili hospitali ipate kufunguliwa na hatimaye kuondoa kero kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali kadhalika wananchi wamejitahidi sana kujenga kwa kujitolea zahanati na vituo vya afya. Hata hivyo tunakabiliwa na matatizo mawili ambayo ni wataalamu, madaktari, wahudumu wengine wa afya pamoja na vitendea kazi. Tunaiomba Serikali katika mgao wa wahudumu na vitendea kazi itufikirie ili nguvu za wananchi walizojitolea katika kujenga ziwe na manufaa kwao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunacho Kituo cha Maendeleo ya Wananchi Mamtukuna. Chuo hiki ni muhimu sana lakini kunakwamishwa na matatizo ya uhaba wa wataalamu (wakufunzi), uchakavu wa majengo, maji pamoja na bajeti ndogo. Tunaiomba Serikali isikiache chuo hiki ikitengee fedha za kutosha walau kutatua kwa awamu matatizo haya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi sasa kumezuka mtindo wa kuwadhalilisha sana watoto wa kike na wa kiume. Baadhi wanaingiliwa, wanaolewa wakiwa na umri mdogo na kufanyishwa kazi ambazo haziendani na umri wao. Imefikia wakati Serikali ichukue hatua thabiti kuzuia mateso haya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho ni ujenzi wa jengo kwa ajili ya installation ya mashine za kansa katika Hopitali ya KCMC. Hospitali pamoja na wafadhili wameshafanya kazi kubwa sana, gharama ya ujenzi wa jengo hilo ni karibu bilioni sita. Kutokana na kuzidiwa kwa taasisi ya kansa Ocean Road na kutokana na wingi wa wagonjwa na mahitaji ya upimaji kwa wananchi, tunaiomba Serikali kuangalia uwezekano wa kusaidia ujenzi wa jengo hili.