Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi kwa Mheshimiwa Ummy A. Mwalimu (Mb), Waziri, Mheshimiwa Dkt. Hamisi Kigwangalla (Mb), Naibu Waziri na ndugu Katibu Mkuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto zilizopo ni pamoja na vituo vya wazee katika makambi; ni muhimu majengo yao yakarabatiwe, wazee wasiojiweza waingizwe kwenye mpango wa TASAF ili kuipunguzia mzigo Serikali, kuwe na huduma ndogo za upatikanaji wa dawa kwenye maeneo ya makambi angalau duka dogo, kwani uwezo wa kufuata dawa kwenye zahanati ni mdogo, Wizara ishirikiane na TAMISEMI kuhakikisha wanajenga x–reter (kuhifadhi kondo la uzazi) kwenye zahanati na vituo vya afya ni tatizo kwani kwenye vituo hivyo wakazi wengi wanalalamika kuwa mbwa wanachukua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa vyumba vya akina mama wanaokwenda kusubiria kujifungua vipewe kipaumbele kwa kutoa msisitizo, vifaa tiba kwa wazazi na watoto vipewe kipaumbele hasa gloves, dawa za kuzuia damu kutoka kwa wingi, kuwepo na wodi maalum ya kuwalaza wanawake wenye ugonjwa wa saratani mikoani na kupeleka dawa za kupunguza maumivu, elimu iendelee kutolewa kwa ugonjwa wa fistula hususan zahanati na vituo vya afya, ugonjwa wa tezi dume.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napongeza kwa ukarabati wa ujenzi wa wodi ya wanawake ya upasuaji katia Hospitali ya Bombo – Tanga, iko vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Benki ya Wanawake, waandae utaratibu na kupelekwa mikoa yote kwani si Dar es Salaam peke yake au mikoa mikubwa yenye Majiji, hata Tabora tunao uwezo. Kwa kuwa mimi ni mwakilishi ambaye nilitoa shilingi 2,000,000 mpaka sasa sijaona faida yoyote, niombe maelezo ya hisa zangu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.