Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nakushukuru na kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kupata muda huu wa kuchangia humu ndani ya Bunge lako Tukufu. Napenda kutoa pongezi nyingi kwa Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watendaji wa Wizara wote kwa kazi nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya pongezi kwa Serikali napenda kuongelea Benki ya Wanawake. Mheshimiwa Waziri uliniahidi kituo cha mikopo na mafunzo ya ujasiriamali, je, Mheshimiwa Waziri ni lini wanawake wa Mkoa wangu wa Morogoro watapata kituo hiki? Nakuomba sana Mheshimiwa Waziri, wanawake hawa hawapatiwe kituo hiki ili waweze kufaidika na mikopo inayotolewa kwa riba nafuu. Naomba tamko lako kwa hili Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya Morogoro, Wilaya hii haina hospitali, je, ni lini hospitali hii itaanza kujengwa kwa ukamilifu? Mheshimiwa Waziri naomba jibu lako wakati utakapokuwa unatoa majibu. Hospitali hii ya Wilaya itaweza kupunguza vifo vya akina mama na watoto na hasa kina mama wajawazito.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Hospitali ya Ifakara au Kibaoni namuomba Mheshimiwa Waziri ashirikiane na Waziri wa TAMISEMI kusudi matakwa ya Hospitali za Wilaya, zahanati na vituo vya afya yatimizwe. Hospitali hii ya Ifakara Kibaoni kuna tatizo ambalo linawahusu watoto ambao wanazaliwa kabla ya wakati yaani watoto njiti, (pre-mature). Hospitali hii haina chumba maalum kwa ajili ya watoto njiti. Watoto hawa njiti wanalazwa wodini pamoja na wale watoto wanaozaliwa kwa wakati (miezi tisa) na wale watoto waliozaliwa kwa ajili ya kuumwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii si nzuri kwani watoto hawa njiti wanatakiwa uangalizi wa hali ya juu. Mheshimiwa Waziri, nakuomba sana chumba cha watoto hawa njiti (pre- mature) kingejengwa haraka iwekanavyo. Pia ingawa hospitali inatumiwa kama hospitali ya Wilaya lakini ina uhaba wa wataalam, dawa na vitendea kazi pia vitendanishi.

Mheshimiwa Waziri, naomba uiangalie hospitali hii ya Ifakara Kibaoni kwa sababu hasa ya watoto hawa njiti ambao hawana chumba maalum.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro tunaomba jengo la mortuary na theatre, x-ray iliyopo haifanyi kazi vizuri na ni ya muda mrefu. Mortuary ni ndogo pia theatre ni ndogo kufuatana na mahitaji, Mheshimiwa Waziri maombi haya ni ya muda mrefu kama hospitali ya rufaa inapaswa kuwa na x-ray inayofanya kazi vizuri, mortuary na theatre.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu elimu ya lishe, miaka ya nyuma elimu ya lishe ilikuwa inatolewa kwenye kliniki na hasa wajawazito na akina mama wanaonyonyesha. Elimu hii ilihusu vyakula vya mtoto na hasa vyakula vya kulikiza na jinsi ya kunyonyesha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vyuo bado vinatoa watu waliochukua nutrition, naomba tuwatumie kikamilifu licha ya matone ya vitamini A, kuweka virutubisho kwenye unga (fertification), kutoa folic acid etc. Pia Mheshimiwa Waziri tuzidi kuwatumia wataalam hawa kwa upande wa vyakula, kwa namna hii tutapunguza utapiamlo kwa ujumla na vifo vya watoto wachanga na wajawazito. Kwa kusaidiana na Wizara husika waajiriwe kila wilaya/kata mpaka vijijini wapewe vitendea kazi pia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu maendeleo ya jamii, idara hii imesahauliwa, Mheshimiwa Waziri nakuomba jitahidi kuiona na hasa Maafisa Maendeleo ni watu muhimu katika kusukuma maendeleo ya nchi na kwenye makazi yetu. Waajiriwe kimkoa/kiwilaya/kata mpaka Afisa Maendeleo wa Kijiji, namuomba Mheshimiwa Waziri aliangalie vizuri jambo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Bima ya Afya, mpaka Machi 2017 ni asilimia 28 tu ya Watanzania ndio wanaotuma bima ya afya. Mheshimiwa Waziri ni mkakati gani utumike hasa ili watu wote, wanawake, wanaume na vijana waweze kutumia bima ya afya kikamilifu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kila kijiji kuwe na zahanati, kila kata kuwe na kituo cha afya na kila wilaya kuwe na hospitali kwa mujibu wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi. Mheshimiwa Waziri naomba useme ni mkakati gani unatumika/utatumia kukamilisha matakwa haya? Naomba na ninashauri jitahidi za kusaidia Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi itimize jambo hili litapunguza vifo vya watoto na kina mama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Sheria ya Ndoa, naumuomba Mheshimiwa Waziri afanye awezavyo iletwe Bungeni. Nimuhimu sana kwa maisha ya watoto wa kike.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja .