Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kuchangia kuhusu usimamizi wa masuala ya hedhi mashuleni. Mashuleni hakuna wataalam wanaotoa elimu ya masuala ya hedhi wala elimu ya afya ya uzazi ili wanafunzi waweze kupata elimu ambayo itawasaidia kuweza kuepukana na mimba za utotoni kwa kuwa miili yao bado ni midogo kuhimili kubeba mzigo (mimba) ambazo huweza kuleta madhara yakiwemo upungufu wa damu, shinikizo la damu, ugonjwa wa fistula na hata vifo vitokanavyo na uzazi. Nashauri wataalam wa idara ya afya wanaoshughulika na masuala ya outreach services watoe elimu ya masuala ya afya mashuleni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mradi wa uimarishaji wa afya ya msingi kwa kuzingatia matokeo (result based financing); Mkoa wa Simiyu ni moja ya mikoa ambayo mradi huu unatekelezwa kulingana na vigezo vya star rating na tayari kuna baadhi ya zahanati zimepatiwa kiasi cha shilingi 10,000,000 kwa ajili ya kutekeleza shughuli zake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna changamoto ya upungufu wa watumishi, naomba Mkoa huu upewe kipaumbele mara ajira za afya zitakapotoka, pia wapo wahitimu ambao wapo tayari kuajiriwa Mkoa wa Simiyu kulingana na changamoto ya watumishi kuhama mara baada ya kuajiriwa.