Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Nami naomba niungane na wenzangu kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu wake pamoja na watendaji wote wa Wizara ya Afya kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitazungumzia mambo matatu tu, la kwanza upungufu wa watumishi; pili, maboma ya zahanati pamoja na vituo vya afya ambayo yalijengwa kwa nguvu za wananchi pamoja na Serikali ambayo hayajakamilika, lakini la mwisho, itakuwa ni kuhusu maendeleo ya jamii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza, mwaka wa jana Mheshimiwa Waziri alitembelea Mkoa wa Kigoma, alipitia karibu Wilaya zote na aliweza kujionea matatizo yaliyopo Kigoma. Mkoa wa Kigoma umekumbwa na wimbi kubwa la wakimbizi waliotoka Burundi, DRC kuja Kigoma, kwa hiyo watu ni wengi sana, wapo watu ambao wako makambini. Kama unavyojua binadamu huwezi kumzuia, wapo wakimbizi wengine ambao wamezagaa katika Wilaya zetu. Kwa maana hiyo basi, katika hospitali zetu watu ni wengi sana,


kwa hiyo tuna kila sababu ya kuongezewa Madaktari na Manesi ili kuweza kukabiliana na tatizo kubwa la wagonjwa ambao ni wengi katika hospitali zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, limekuwepo tatizo la watumishi. Karibu nchi nzima kumekuwa na kilio kwamba watumishi hawatoshi, sasa kutokana na tatizo hili la vyeti lililojitokeza tatizo la watumishi litakuwa ni kubwa sana. Kwa hiyo naomba Serikali ijipange haraka iwezekanavyo kuhakikisha inapeleka watumishi wa afya katika Wilaya zetu na hususani huko vijijini, la sivyo wananchi watapoteza maisha kwa wingi sana kwa sababu hakutakuwa na Wauguzi na Madaktari. Kwa hiyo, tunaomba Serikali ijipange kuhakikisha watumishi wanapelekwa katika maeneo hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika ilani yetu ya CCM tulisema tutajenga zahanati pamoja na vituo vya afya na wananchi kwa kushirikiana na Serikali wameshajenga maboma ya zahanati na vituo vya afya. Hata hivyo kumekuwa na kilio cha muda mrefu kwa ajili ya maboma yale, kwamba, yanabomoka na hayana msaada wowote. Kwa hiyo, naomba Wizara kwa kushirikiana na TAMISEMI waweze kuliangalia hili ili yale maboma yaliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi na Serikali kwa maaana ya zahanati na vituo vya afya yaweze kukamilika kusudi huduma…

KUHUSU UTARATIBU....
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa
Mwenyekiti, nashukuru kwa kumwelimisha huyu ni Mbunge mgeni mimi ni senior. Naomba niendelee na mchango wangu. Naamini Wizara ya Afya pamoja na Wizara ya TAMISEMI wakikaa pamoja tutafanikiwa kuweza kupata majengo ya zahanati na vituo vya afya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie kuhusu Maendeleo ya Jamii. Maendeleo ya Jamii yamesahaulilka, nakumbuka siku za nyuma, enzi za mwalimu Mabibi Afya walikuwa wanatembea katika vijiji kuhamasisha shughuli za maendeleo na wananchi walikuwa wanaelimika kwa kupitia mabibi maendeleo. Sasa naomba kwamba maendeleo ya jamii wapewe vitendea kazi, tofauti na sasa hivi wako chini ya Mkurugenzi, Mkurugenzi akipata makusanyo ndipo anawapatia pesa kidogo ndio wanakwenda kufanya uhamasishaji wa shughuli za maendeleo vijijini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba, kwa kutumia Bunge lako Tukufu niwapongeze wa Wakurugenzi wa Wilaya ya Kasulu, Kibondo na maeneo mengine ya Mkoa wa Kigoma kwa kuweza kutimiza kwa kupeleka asilimia tano kwa vijana na wanawake. Kwa sababu hiyo, naomba sasa juhudi ziongezeke kusudi pesa hizo ziwe zinapelekwa kuweza kuwasaidia wanawake na vijana. Na watasaidiwaje basi, ni kwa kuungana na watendaji pamoja na hawa watu wa Maendeleo ya Jamii kwenda kuhamasisha wanawake na vijana kuanzisha vikundi ili ile asilimia tano inayotolewa ya vijana na wanawake iweze kupelekwa kwenye vikundi hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimalizie kwamba tunafahamu kabisa vipo vituo vipya vya afya ambayo vinajengwa ambavyo kwa sasa hivi kwa mfano kule Wilaya ya Kasulu vipo vituo vipyaa vinavyojengwa… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.