Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Lathifah Hassan Chande

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. LATHIFAH H. CHANDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa ya kuchangia kwenye Wizara hii ya Afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuongelea juu ya sera ya Serikali ya kuhakikisha kila kata nchini inapata kituo cha afya. Mpaka sasa hivi imeonesha hii sera imeshindikana na kupelekea katika kata za nchi nzima 3,959, kata 448 tu ndiyo zimepata vituo vya afya. Sasa tukienda kwenye Mkoa wa Lindi, tuna kata 138 lakini cha kusikitisha sana ni kata 19 tu ambazo zina vituo vya afya. Kibaya zaidi ni kata moja tu yenye kituo cha afya ambacho kinatoa huduma ya dharura ya upasuaji ya mama mjamzito, hii kata iko Kilimalondo - Nachingwea. Hii imepelekea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Lindi kuwa tegemezi kubwa kwa ajili ya kutoa huduma ya afya especially kwa akina mama wajawazito.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu kibaya zaidi na kutegemewa kote kwa hii hospitali ukiangalia majengo yake tangu mwaka 1954 hayajawahi kufanyiwa ukarabati wowote. Vilevile hakuna nafasi ya kutosha, hata tukisema pawe expanded palepale kibaya zaidi labour ward ina uwezo wa kuhudumia akina mama wajawazito 30 tu kwa wakati mmoja wakati wa kujifungua, hii ni hali mbaya sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile vifaa muhimu kama x-ray hakuna, sasa hivi ni miezi mitatu ilikuwepo x-ray moja tu ambayo mpaka sasa hivi haifanyi kazi, kwa hiyo hilo pia liangaliwe. Pia watumishi hawatoshelezi mahitaji ya hospitali ile ya Mkoa. Wauguzi wengi wamestaafu, hakuna specialists wa kutosha na hii tumbua tumbua yenu hii kwa maana hiyo hata hao wachache waliopo tumbua tumbua kwa sababu ya kutuaminisha kwa ajili ya kuwa na vyeti fake, matokeo yake hawa wachache pia wataendelea kupungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa Serikali ihakikishe inatekeleza sera yake ya kuhakikisha kila kata inafikiwa na kupatikana vituo vya afya katika hizo kata, pia kutokana na kwamba tayari kuna eneo limetengwa kwa ajili ya kujenga Hospitali ya Mkoa wa Lindi, basi kwa nini Serikali
isifikirie angalau unit ya labour iweze kuwepo pale, ambayo itakuwa na facilities zote zinazohitajika kwa ajili ya mama anapokuwa anajifungua, hii itasaidia kupunguza hata maternal mortality rate. Pia kuweza kuajiri watumishi zaidi watakaoweza kukidhi mahitaji yaliyopo pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu bima ya afya, takwimu zinaonesha kwamba ni asilimia nane tu ya Watanzania ambao wako kwenye mfumo wa bima ya afya, ni dhahiri mnafahamu ni mzigo kiasi gani wa gharama uliyopo kwa wananchi juu ya huduma hii ya afya. Napenda kuishauri Serikali iweze kupunguza tozo zisizokuwa za msingi ili hata private sectors waweze kutoa huduma hii ya afya kwa gharama zilizo nafuu ili wananchi waweze kufikiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vifaa tiba na dawa; Serikali imekuja na mfumo ambao uko centralized, ambapo dawa zote zinasambazwa na Medical Stores Departments, ni dhahiri kwamba usambazwaji wa dawa kikamilifu umeshindikana, maeneo yote yanashindikana kufikiwa…(Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. LATHIFAH H. CHANDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.