Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Abdulaziz Mohamed Abood

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. ABDUL-AZIZ M. ABOOD: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii.

Kwanza nichukue nafasi hii kuipongeza Serikali yangu ya Awamu ya Tano kwa kazi nzuri inayoendelea kuifanya. Pia nimpongeze Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri kwa kazi nzuri wanayoendelea kuifanya katika kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye bajeti ya mwaka 2016/2017 niliwahi kumwambia Mheshimiwa Waziri kuhusu matatizo ya hospitali ya Mkoa wa Morogoro, kuhusu x-ray machine, majokofu ya kuhifadhia maiti na upungufu wa madaktari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitakuwa mchoyo wa fadhila iwapo nisipomshukuru Waziri na Naibu Waziri. Walishughulikia tatizo ya x-ray machine, walitutumia Wataalam ambao machine yetu ilikuwa ni analogue wakaibadilisha kuwa digital na sasa inahudumia wagonjwa 50 mpaka 70 kwa siku. Pia tumeweza kuunganishwa katika mfumo wa tele-medicine ambao wanapata ushauri zaidi kwa Madaktari Bingwa.

Kuhusu majokofu tunamshukuru Mheshimiwa Waziri ametupatia na sasa katika wiki hii yanaanza kutolewa ya zamani na kuwekwa mapya katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro. Upungufu wa madaktari tunashukuru Mheshimiwa Waziri umetutimizia kiasi kikubwa ila tuna tatizo bado moja kubwa la specialist wa ENT ambaye hatuna hata mmoja.

Pili, tuna tatizo vilevile la wafamasia ambao walitakiwa wawe 14 lakini tunae mmoja tu msaidizi. Kwa hiyo, tunaomba Mheshimiwa Waziri katika hilo naamini kwa kazi unazozifanya na Naibu Waziri kwa speed ya Awamu ya Tano mtatumalizia kero hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kero nyingine ni wodi ya wazazi katika hospitali ya Mkoa wa Morogoro. Hospitali ya Mkoa inapokea wazazi 40 kwa wastani kwa siku na wodi inaweza kupokea wagonjwa 20 mpaka 25 tu kwa siku. Kwa hiyo, tungeomba Mheshimiwa Waziri atuongezee wodi nyingine katika bajeti yake ili tuweze kutimiza mahitaji ya wazazi katika wodi hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kero nyingine tuliyonayo Morogoro ni ambulance. Tunayo ambulance moja tu na wagonjwa wanakuwa ni wengi mno kiasi ambacho wengine wanaandikiwa rufaa ya kwenda Muhimbili, ambulance moja inashindwa kufanya kazi yake. Kwa hiyo, tunakuomba Mheshimiwa Waziri uliangalie hilo na nitakupa ushirikiano ili tuweze kupata ambulance mpya nyingine kwa ajili ya hospitali ya Mkoa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna tatizo lingine la gharama za wanaovunjika viungo kwa maana ya wanaovunjika mifupa kwenye ajali na matatizo mengine. Gharama zile katika Hospitali ya Mkoa ambao hawana bima ya afya ni kubwa mno kuanzia shilingi 500,000 mpaka shilingi 700,000, lakini ukiuliza unaambiwa kwa sababu ya gharama ya vyuma.

Kwa hiyo, tunakuomba Mheshimiwa Waziri uliangalie hilo kwa sababu gharama hizi kwa watu wa hali ya chini wanashindwa kumudu, tungeomba mtufikirie juu ya hili ili tuweze kupata vyuma na vifaa vingine kwa ajili ya kuweza kupunguza gharama hizo ili wananchi waweze kugharamia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho nakushukuru kwa kunipa nafasi hii. Ahsante sana, naunga mkono hoja.