Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Munde Abdallah Tambwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa hii niweze kuchangia. Dakika tano ni chache yaani leo nitaacha hata kukisifia chama changu na Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa naomba nichangie moja kwa moja matatizo yangu ya Mkoa wa Tabora. Mkoa wa Tabora tuna Chuo cha Waaguzi pamoja na Madaktari, nimeongea hapa Bungeni mara kadhaa. Mheshimiwa Naibu Waziri amekwenda Tabora kufuatilia, akatoa maagizo kwamba Katibu Mkuu atakuja, Katibu Mkuu hakwenda Tabora, wakaenda Maafisa watatu tarehe 27 Januari, wakasema watarudi lakini mpaka leo hii hawajarudi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pesa za walipa kodi zimefanya kazi kubwa, mpaka napoongea hapa chuo kimefikia stage ya magodoro na vitanda, theatre imekamilika kwa mashine zote, kasoro mitungi ya hewa tu lakini mkandarasi amefunga, ufunguo anao yeye, hata Naibu Waziri alivyokwenda amechungulia dirishani hakuweza kuingia. Ni asilimia kumi tu zimebaki, kwenye chuo ni tape za mabomba na kwenye theatre ni mitungi ya hewa lakini hela ya walipa kodi inapotea bure, jengo lile limegeuka kuwa gofu, linaharibika, value for money imepotea.

Mheshimiwa Waziri utakapokuja hapa uje uniambie kuhusu status ya Chuo cha Manesi na Madaktari wa Tabora. Kwa kweli hizi hela za walipa kodi zinapotea hivi hivi huku mkiziangalia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa haraka haraka naomba niongelee Hospitali ya Wilaya ya Tabora Manispaa. Tabora Manispaa tumeanzisha jengo la Hospitali ya Wilaya miaka mitatu sasa, tulitenga shilingi milioni 150, tukatenga shilingi milioni 120 lakini Serikali Kuu haijatuunga mkono. Tunamuomba sana Mheshimiwa Simbachawene, Mheshimiwa Ummy, najua hizi Wizara zinaingiliana mtusaidie kuhusu Hospitali ya Wilaya ya Tabora Manispaa. Msongamano katika Hospitali ya Mkoa ni mkubwa sana, Wilaya ya Tabora Manispaa ina population ya watu zaidi ya 400,000 bila kuwa na Hospitali ya Wilaya hatutaweza kabisa kumudu hali hii. Tutabaki tunailaumu Serikali kila siku lazima tuwe na Hospitali ya Wilaya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya Uyui pia wameanza kujenga jengo lao la ghorofa lakini wameshindwa kumalizia tu. Tunaomba muwa-support nao wapate Hospitali ya Wilaya ili kuondoa msongamano mkubwa kwenye Hospitali ya Mkoa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Ummy bajeti iliyopita alituahidi mikoa yote ya pembezoni atapeleka Madaktari Bingwa. Ninavyoongea hapa Hospitali ya Mkoa wa Tabora kuna Madaktari Bingwa wawili tu badala ya 34. Kuna daktari wa mifupa na daktari wa wanawake alioazimwa kwenye Manispaa. Tunaomba mtupelekee Madaktari Bingwa sisi tulioko pembezoni kwani nako pia kuna Watanzania wanaohitaji huduma za hospitali. Muhimbili madaktari wamejaa tele, lakini huku kwenye hospitali zetu hakuna. Mheshimiwa Waziri alituahidi naomba anapokuja kutujibu atuambie kuhusu suala hili la upatikanaji wa Madaktari Bingwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Nursing Officer tunahitaji 37 lakini tunao watatu tu, tunahitaji Assistant Nurse 131 tunao 82, wauguzi wenye certificate tunahitaji 147 tunao 44, hatimaye wodi kubwa wenye watu 80 analala nurse mmoja atahudumiaje watu, tutakuwa tunalaumu ma-nurse lakini tatizo kwa kweli lipo. Haiwezekani nurse mmoja akahudumia watu 80, mmoja drip imeisha, mwingine anataka kujisaidia, mwingine muda wa sindano umefika, matokeo yake wanaona kama ma-nurse hawawasaidii watu, lakini kwa kweli ma-nurse ni wachache wagonjwa ni wengi sana. Mheshimiwa Ummy tunakuamini naomba na sisi uendelee kutunza imani yako kwetu, hili jambo ni kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee tena suala la x- ray ya Nzega, Wabunge wote wa Nzega wameongea. Mimi niseme tu Phillips anadai hela zake Mheshimiwa Ummy tuambie unamlipa lini hela zake atengeneze x-ray ya Nzega, tusipindishe maneno. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee Benki ya Wanawake. Mheshimiwa Ummy uliahidi utakuja…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naunga mkono hoja.