Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. DR. ANGELINA S. L. MABULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuunga mkono hoja. Ombi langu wananchi wa Kata ya Kanyerere na Kata jirani katika Wilaya ya Magu wana tatizo kubwa la usafiri kuweza kufikia visiwa vya base (Ilemela) na kisiwa cha Mashoka – Magu. Katika Kikao cha RCC kilichofanyika Mkoa wa Mwanza Januari, 2017, waliahidi kupeleka kivuko baada ya kufanya tathmini ya abiria, mizigo na shughuli za kiuchumi zinazofanyika katika visiwa hivyo na kuona vinastahili kuwa na kivuko. Ombi langu ni utekelezaji wa ahadi hiyo.

(1) Barabara ya Sabasaba - Kiseke hadi Buswelu ilikuwa ahadi ya Waziri alipotembelea Jimbo langu, naomba barabara hiyo kuwa ni kiungo cha Makao Makuu ya Wilaya na Kata zaidi ya saba ijengwe. Aidha, barabara hiyo itarahisisha pia kuwa kama mchepuko wa wasafiri waendao Mara na Shinyanga.
(2) Barabara ya Airport, Kayenze hadi Nyanguge nayo pia itasaidia mchepuo kuelekea Mara na Serengeti katika Mbuga za Wanyama na kuchochea utalii katika maeneo hayo.
(3) Tunahitaji minara ya simu katika Kata ya Kayenze na Sangabuye hawana mawasiliano ya uhakika katika baadhi ya mitaa ya Kata hizo za Kabusungu, Igumamoyo, Imalang’ombe na kadhalika.