Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Wizara kwa jinsi inavyotekeleza vema Ilani ya Chama cha Mapinduzi. Nampongeza Waziri na Naibu Waziri kwa utekelezaji wa majukumu yao. Pamoja na hayo nachangia yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naishukuru Serikali kwa kutenga fedha za ujenzi wa gati mita 300 shilingi bilioni 87, pia ujenzi wa gati la mafuta Shangani. Aidha, ukarabati wa gati Na. 3 tunaomba fedha hizo zitolewe kwa wakati ili miradi hiyo itekelezwe kwa muda uliopangwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami Mtwara- Newala- Masasi kipande cha kilomita 50, Mtwara- Mnivate, Mkataba wa kazi hii ni miaka miwili na thamani yake ni zaidi ya bilioni 90. Kwa fedha zilizotengwa bajeti ya mwaka jana na mwaka huu fedha zilizotengwa ni takribani shilingi bilioni 29, hivyo kama Mkandarasi atafanya kazi kwa nguvu zote na kasi kubwa hakutakuwa na fedha za kumwezesha. Naomba angalizo hili lifanyiwe kazi ili barabara hiyo ijengwe kwa muda uliopangwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mawasiliano ya simu. Katika Jimbo la Nanyamba kuna Kata nyingi ambazo hakuna mawasiliano ya simu. Baadhi ya Kata hizo ni Njengwa, Nitekela, Nyundo, Hinju, Mnima, Kiromba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niliuliza swali Bungeni kuhusu lini Kata hizo zitapewa mawasiliano ya simu, nikajibiwa kuwa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) utagharamia ujenzi wa minara katika maeneo hayo. Naomba tena kupitia Mfuko huu kuharakisha ujenzi wa minara katika maeneo hayo ili kuwe na mawasiliano ya simu za mkononi.