Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Sixtus Raphael Mapunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia jioni hii ya leo. Awali ya yote, naomba nichukue fursa hii kumshukuru na kumpongeza Waziri Mkuu kwa jinsi alivyoitoa hotuba yake kwa umahiri na ufundi mkubwa, iliyogusa kila sekta. Hakika hotuba hii ime-reflect katika maana ya utendaji, hotuba iliyotolewa na Mheshimiwa Rais siku analizindua Bunge.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hotuba ya Waziri Mkuu imegusa mambo mengi ambayo kama hayo yote tutakwenda kuyafanyia kazi kama alivyoyawasilisha hapa, nina uhakika ndani ya miaka michache nchi yetu itakuwa katika kiwango cha hali ya juu sana cha maendeleo. Niwaombe Mawaziri wote, kadiri Waziri Mkuu alivyoeleza kwenye hizo sekta, tuziongezee nguvu ili maendeleo kwa Watanzania yapatikane kwa haraka. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na haya mambo yote mazuri ambayo Mheshimiwa Waziri Mkuu ameyaeleza, kuna maeneo machache naomba nijikite ili kuiomba Serikali iongeze nguvu sana ili tuweze kuendelea kwa wakati.
Jambo la kwanza ameelezea nishati ya umeme. Umeme ni jambo muhimu sana kwenye maendeleo ya Taifa lolote lile. Tuko kwenye mfumo wa gesi na aina nyingine zote za umeme ambazo zimewekwa katika programu ya mwaka 2016/2017. Niwaombe sana mtusaidie na sisi watu wa Songea katika maana ya Mkoa wa Ruvuma kama mlivyoeleza kuweka mfumo mpya wa umeme wa gridi ya Taifa kilowatt 220 kutoka Makambako Songea na nina imani hautaishia Songea utafika Mbinga utakwenda mpaka Nyasa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ni suala la viwanda. Suala la viwanda ni zito na ni kubwa sana na ni moja kati ya sera ya Awamu hii ya Tano. Kama tutawekeza kwenye viwanda hasa vile viwanda ambavyo vilisinzia na vingine vilikufa au vingine vinafanya kazi chini ya kiwango, nina uhakika ajira itapatikana kwa vijana na maendeleo makubwa yatapatikana kwa nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kule Mbinga tuna kiwanda cha kahawa. Niiombe Serikali ikitazame kile Kiwanda cha Kahawa Mbinga na kiende hatua ya pili sasa kuweka kiwanda kingine cha Instant Coffee ili kahawa ile ikishakobolewa siyo lazima tuipeleke Brazil, India au Ujerumani, tutengeneze pale pale kahawa na sasa tuwe na kahawa made from Mbinga. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nataka niliongelee ni suala la afya. Kati ya changamoto ambazo zinatukabili kule Mbinga ni Hospitali yetu ya Wilaya. Hospitali yetu ya Wilaya ilianzishwa kama kituo cha afya. Kwa bahati nzuri maendeleo ya Mji wa Mbinga yakapelekea kuwa na Wilaya ya Mbinga ambayo baadaye ikazaa Wilaya ya Nyasa. Hata hivyo, hizi wilaya zote mbili, Wilaya ya Mbinga na Nyasa zinategemea Hospitali ya Wilaya ya Mbinga, Hospitali ya Mbuyula ambayo kwa sasa inahudumia Halmashauri nne za Nyasa, Mbinga Vijijini, Mbinga Mjini na sehemu ya Halmashauri ya Songea Vijijini. Niombe sana Serikali iwekeze kwenye ile hospitali ili tuweze kuwasaidia wananchi wetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sehemu nyingine ninayoomba Serikali iongeze nguvu ni kwenye huduma ya maji safi na salama. Ule mji unakua kwa kasi sana lakini mpaka sasa hatuna mradi mkubwa wa maji wa kuweza kuwasaidia wananchi wa Mbinga wanaoongezeka siku mpaka siku.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kuipongeza hotuba nzuri sana ya Waziri Mkuu, nimepata muda kidogo kuisoma hotuba ya Kambi ya Upinzani. Hii hotuba ya Waziri Mkuu ina page 82, imegusa kila maeneo, hii iliyowasilishwa na Mheshimiwa Freeman Mbowe ina vi-page kama tisa vile, font ni kubwa sana na double space, haiwezi hata kidogo ikajibu hoja ya page 82. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ukiondoa hayo, ameiwasilisha hoja hii na amepotosha watu hapa kana kwamba watu hawasomi au hawafikiri. Nimwombe Mheshimiwa Mbowe akasome mambo yafuatayo. Kwanza, akaisome vizuri Katiba aielewe, akishaielewa vizuri akasome Sheria ya Bajeti, halafu vile vile akasome na Appropriation Act ya mwaka 2015. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, unapoongelea kutengeneza bajeti lazima uweke sheria itakayosimamia utekelezaji wa bajeti ile na sheria hiyo inaitwa Appropriation Act. Kwa muktadha wa shughuli yetu ya leo ile Appropriation Act ilikuwa ya mwaka 2015 ambayo ina section sita au kwa lugha nyingine ina vifungu sita. Katika vile vifungu sita kuna kifungu cha 6 kinasema mamlaka ya Serikali kubadilisha matumizi kadiri itakavyoona inafaa kwa maslahi ya Taifa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu Mheshimiwa Mbowe alinukuu vipengele vya Katiba sasa mimi nimuambie Katiba ni sheria mama, inatafsiriwa kwenye sheria na ukitoka kwenye sheria ukafika kwenye bajeti utekelezaji wa bajeti unakwenda kwenye Appropriation Act. Sasa mimi nampeleka kwenye Appropriation Act ya mwaka 2015, kifungu cha sita (6) kinachosema, power of the Minister to reallocate certain appropriated moneys. Imeelezea kifungu cha kwanza (1) mpaka cha tano (5) ila kwa faida ya kikao hiki mimi nakisoma vizuri kifungu kile cha tano (5), kinasema hivi, nanukuu:-
“The Minister may, by certificate under this hand, reallocate any sums arising from savings in the Consolidated Fund to any of the purposes specified in the second, third and fourth columns respectively of the Schedule to this Act, and where this occurs, the provisions of section 3 and 4 shall take effect as if the total sum granted out of the Consolidated Fund and the amounts appropriated for the purpose specified in such certificate were raised by the amount or amounts specified in the certificate”.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa anachotuambia hapa ni nini? Anachotaka kutukoroga hapa ni nini?
MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbowe aliongea kwa Kiingereza, mimi najua alikuwa na maana ya kupotosha watu wasielewe Kiingereza. Kwa Kiswahili kisichokuwa rasmi, Waziri ana mamlaka kwenye hii Sheria ya Bajeti tuliyoipitisha kwa maslahi ya nchi anaweza akaondoa kifungu kimoja under certificate kwa matumizi mengine yenye muktadha ule ule unaofanana kwa maendeleo ya nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kuchukua pesa ambayo ilibaki kwenye matumizi from July, August, September, October ambapo Bunge halikuwepo tukaenda kununua madawati kwa mujibu wa sheria aliyetunga yeye mwenyewe na alikuwa amekaa pale, leo anajidai kasahau, huku kujisahaulisha kunatokana na nini? Niwaombeni, watu kama hawa tuwaangalie vizuri wenye ndimi mbilimbili, huku unauma huku unapulizia…
MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Unafikiri sisi wote hapa ni matutusa? Humu hakuna zero, watu tunafikiri kwa kutumia vichwa, hatufikirii kwa kutumia matumbo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.