Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ujenzi; Mheshimiwa Waziri kwa masikitiko makubwa sana Mkoa wa Lindi mwaka huu mmeupatia fedha chache kuliko uhalisia wa miundombinu iliyopo. Kwa nini Lindi, mkoa mkubwa kwa eneo tena bado miundombinu yake bado haijaimarika, unatengewa fedha chache kuliko mkoa wenye eneo dogo kama vile Kilimanjaro ambao umetengewa kiasi cha fedha zaidi ya trilioni 2.2 wakati Mkoa wa Lindi mmeutengea fedha chache kiasi cha shilingi bilioni 800 tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini Jimbo la Mchinga ambalo mimi ni Mbunge wake halijatengewa fedha hata senti moja katika fedha za maendeleo, kwa nini mgao wa rasilimali za nchi hii hauzingatii usawa kwa sehemu yote ya nchi hii? Naomba maelezo ya kina juu ya swali hili.