Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. DKT. MEDARD M. KALEMANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika miradi ya barabara za Mikoa inayotengenezwa kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara kwa mwaka wa fedha wa 2017/2018, barabara kwa ajili ya upgrading to DSD Mkuyuni kutoka Chato Mjini, eneo la Mkuyuni imewekwa kilometa nne tu. Ukweli ni kwamba barabara hii ina urefu wa kilometa 18 kutoka Chato Mjini kupitia Mkuyuni, Rubambangwe JCT, Kanyama, Ilemela hadi Busarara. Barabara hii inaunganisha barabara inayotoka Nyamilembe hadi Katoke inayoungana na barabara ya Biharamulo kuelekea Bukoba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa barabara hii ni muhimu katika kuunganisha barabara kuu ya kwenda Biharamulo na Bukoba na kwa kuwa, ilikuwa katika sehemu ya ahadi za Serikali tangu Bunge la Kumi katika miaka ya 2013/2014, naomba sasa ijengwe kama ilivyotarajiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika ukurasa 285 katika jedwali la barabara zilizotengewa fedha kwa kiwango cha lami barabara hii inaonekana kuwa kilometa nne tu ndizo zitakazojengwa kwa gharama ya millioni 300 pamoja na kwamba barabara hii haiishii hapo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa barabara hii ni mwendelezo wa kilometa nne zilizotajwa katika bajeti ya Wizara zinaishia njiani katika JCT ya Rubambungwe na kuiacha sehemu kubwa bila kujengwa kwa kiwango cha lami. Naiomba sasa Wizara ya Uchukuzi, Ujenzi na Mawasiliano waingize sehemu nzima ya barabara hii yenye jumla ya kilometa 18 ili ijengwe kwa kiwango cha lami katika mwaka huu wa bajeti 2017/2018, badala ya kujenga kilometa nne tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia wakati Mheshimiwa Waziri anahitimisha hoja asisitize kuwa barabara hii itatekelezwa ili wananchi wa maeneo haya na maeneo jirani wapate unafuu wa kufanya shughuli zao za kiuchumi kwa kuwa na usafiri rafiki na rahisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.