Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. January Yusuf Makamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bumbuli

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. JANUARY Y. MAKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nawapongeza Viongozi Makatibu Wakuu wa Wizara na Watendaji wa Taasisi zilizo chini ya Wizara, ikiwemo TANROADs kwa kazi nzuri mnayoifanya. Kazi inaonekana na jitihada pia zinaonekana. Kwa miaka zaidi ya 20 sasa wananchi wa Kongowe na Bumbuli wamekuwa wanangoja barabara ya kwanza ya lami katika eneo hilo. Wamekuwa wanaipigia kura CCM kwa matumaini hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, ahadi ya barabara ya kutoka Soni – Bumbuli – Kwashemshi – Korogwe kujengwa kwa kiwango cha lami bado imebaki ahadi ya kwenye Ilani na kwenye Kauli za Viongozi. Wananchi hawa sasa wanakata tamaa. Mwaka jana kwenye vitabu vya bajeti barabara hii ilionesha sifuri, yaani haikupangiwa fedha. Jambo hili lilitusikitisha. Mwaka huu tumeona fedha kidogo sana kwa ajili ya kumalizia design kwa kipande cha mwisho. Naomba na kupendekeza kwamba, kwa kuwa kipande cha Soni – Bumbuli tayari design imefanyika, fedha zipangwe kuanza angalau kilomita 10 za lami mwaka ujao wa fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara za kupandishwa madaraja kuwa za TANROADs; vilevile tulipendekeza barabara mbili na kuzipitisha katika michakato yote husika kwa ajili ya kupandishwa madaraja. Barabara hizo ni: Kwanza, barabara ya Soni - Baga – Ngwashi – Milingano – Mashawa na pili ni Soni – Mponda – Tawota – Keronge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hizi zinaunganisha Wilaya na Majimbo matatu. Tunasubiri majibu ya Wizara kwa maombi haya.