Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Hamadi Salim Maalim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kojani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. HAMAD SALIM MAALIM: Mheshimiwa Mwenyekiti, naanza hoja yangu kwenye suala zima la viwanja vya ndege. Viwanja vya ndege si suala la Muungano lakini ndani ya viwanja vya ndege mna mambo ambayo ni ya Muungano. Suala la anga ni suala la Muungano na kwa maana hiyo utendaji wake wa kazi pia utakuwa uko chini ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuondosha sintofahamu ya utendaji kwa section hii kwa upande wa Zanzibar ningeomba Wizara husika ikaliangalia suala hili kwa kina na baadaye kupeleka mapendekezo yao kwa Serikali ya Muungano ili suala hili kwa upande wa Zanzibar libakie kama suala la Zanzibar na utendaji wake usimamiwe na SMZ.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya suala hilo sasa naomba niende moja kwa moja kwenye suala la bandari. Wafanyabiashara kwa mfano wanaoleta magari kutoka nje ya nchi na kuyateremsha kwenye Bandari ya Zanzibar hulazimika kuyalipia magari hayo kodi zote zinazostahilil. Hata hivyo, mfanyabiashara huyo huyo akiamua sasa kusafirisha gari hilo na kulipeleka Tanzania Bara pia hulazimika kulipia kodi mbalimbali Bandarini Dar es Salaam. Je, hatuoni kwamba kufanya hivyo ni kuwarudisha nyuma wafanyabiashara hao?

Mheshimiwa Mwenyekiti, si hayo tu bali hata gari iliyonunuliwa Zanzibar na baadaye kusafirishwa kupelekwa Tanzania Bara basi ushuru wake ni mkubwa sana, kwa nini hali iwe hivyo na hii yote ni nchi moja? Nashauri hili liangaliwe ipasavyo ili kuwaondolea wafanyabiashara ugumu wa biashara.