Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Jenista Joackim Mhagama

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Peramiho

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. JENISTA J. MHAGAMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naungana na wenzangu kuunga mkono hoja. Nampongeza sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Makatibu Wakuu na timu nzima ya Uongozi wa Wizara. Napongeza uamuzi wa Serikali wa kuanzisha safari za ndege Songea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maombi ya Jimbo la Peramiho:
(i) Kupandisha hadhi barabara ya Tulila-Chipole- Matomonda kuwa ya Mkoa kwa sababu inaunganisha Wilaya mbili lakini ni barabara inayotupeleka katika mradi mkubwa sana wa umeme wa maji unaotumika Songea.
(ii) Barabara ya Mkenda-Likuyufusi. Barabara hii inatajwa katika Ilani ya Uchaguzi, ni barabara inayotuunganisha na Nchi ya Msumbiji, ni barabara ya Taifa. Upembuzi yakinifu umekamilika, usanifu tayari japo ni muda mrefu sana sasa, naomba sana tuanze kuweka lami japo kilomita 15 tu kuanzia ulipo mpaka wa Tanzania na Msumbiji.
(iii) Barabara ya Mpitimbi-Ndongosi ni ya mpakani na inahudumiwa na Mfuko wa Barabara Mkoa. Tunaomba tutengewe fedha.
(iv) Barabara ya Mkoa ya Mletewe-Matimila- Mkongo ya Mkoa haijatengewa fedha muda mrefu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.