Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon Faida Mohammed Bakar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. FAIDA MOHAMMED BAKAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja kwa asilimia mia moja pamoja na kumpongeza Mheshimiwa Waziri wa Wizara hii kwa kazi nzuri azifanyazo akishirikiana na Naibu Waziri wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia kuhusu miundombinu ya mitandao ya simu katika Kisiwa cha Pemba. Kwa kuwa Kisiwa cha Pemba mtandao unaopatikana kwa urahisi katika maeneo mengi na hasa vijijni hususani mtandao wa TiGO haupatikani vizuri. Naiomba Serikali kupitia Wizara hii iweze kulishughulikia suala hili la mtandao wa TiGO uweze kuenezwa sehemu zote katika kisiwa hiki kwa kuwa mitandao husaidia sana wananchi na hasa wafanyabiashara katika mawasiliano ya haraka na ya karibu. Naishauri Serikali kulishughulikia tatizo hili la mtandao wa simu katika Kisiwa cha Pemba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia niongelee kuhusu viwanja vya ndege. Pamoja na Serikali kuviimarisha viwanja vya ndege katika nchi hii sambamba na Serikali kununua ndege za kisasa za kuhudumia wananchi wake, napenda kuomba Serikali iendelee kukifanyia ukarabati mkubwa Kiwanja cha Ndege cha Pemba na zaidi kukipanua ili kukidhi huduma ya kupokea ndege kubwa za kisasa pamoja na kuziwezesha ndege hizi kuruka na kutua muda wote wa mchana na usiku. Wananchi wa Pemba wanapendelea sana kutumia ndege kwa ajili ya safari za kijamii na kibiashara, naomba marekebisho yafanywe katika kiwanja hicho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.
Ahsante.