Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. FREDY A. MWAKIBETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kunipa fursa hii ya kuweza kuchangia kwenye Wizara hii kwa mwaka wa fedha 2017/2018.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Busokelo lipo Mkoa wa Mbeya, Wilaya ya Rungwe. Kwa bahati mbaya sana miundombinu ya barabara haipo vizuri. Jimbo hilo tunalima mazao mbalimbali, kwa mfano, ndizi, kokoa, chai, viazi mviringo na vitamu, mihogo, mahindi, ufugaji wa ng’ombe wa maziwa, kilimo cha matunda, maparachichi, upasuaji wa mbao na shughuli zingine mbalimbali. Hata hivyo, miundombinu ya barabara ni mibovu sana, imesababisha mazao mengi kuoza, kuharibikia shambani na hivyo kuwafanya wananchi wa Busokelo kuwa maskini kwa sababu ya barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara tunazoomba kupandishwa hadhi ziwe chini ya TANROAD Mkoa wa Mbeya ni zifuatazo:-
(i) Barabara ya Lwangwa – Tiete-Lufilyo (kilomita15).
(ii) Barabara ya Kanyelele (Gesi) – Mpata –Ipembe –Suma (kilomita15).
(iii) Barabara ya Kyejo (Gesi) – Lwangwa (kilomita 5.7).
(iv) Barabara ya Lugombo-Bujingijira – Ngumbulu - Mbeya Vijijini (kilomita10).
(v) Barabara ya Itete – Kisegese – Ntaba - Ngeleka - Matema (kilomita 30).
(vi) Barabara ya Kilasi – Kitulo (Livingstone) - Makete (Njombe) (kilomita 30).

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya lami kutoka Katumba (Tukuyu) - Lwangwa - Mbambo Tukuyu, tunaomba sana iendelee kujengwa kwa kiwango cha lami kutoka Busokelo – Isange - Katumba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni muhimu TCRA waweke mifumo ya kukusanya kodi toka kwa mobile operators. Mheshimiwa Mwenyekiti, Uwanja wa Ndege wa Songwe. Uwanja huu ni muhimu sana kwa Nyanda za Juu Kusini. Uwanja unahudumia Mbeya, Njombe, Rukwa, Katavi na Ruvuma pamoja na nchi jirani kama Malawi, Zambia, Congo na nyinginezo. Tunaomba kuwekewa taa za kuongozea ndege, kwa hali ilivyo hivi sasa, ndege haziwezi kutua wakati wa usiku na wakati wa ukungu na hivyo kusababisha hatari kwa abiria na usalama kwa ndege zenyewe. Aidha, naomba jengo la utawala lililopo Songwe limaliziwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuundwa kwa Bodi ya Wanasayansi waliomaliza masomo ya computer Science and Information Technology. Nchi yetu inapita kwenye sayansi na teknolojia. Asilimia kubwa ya pato la Taifa ni kutokana na mifumo ya IT. Napendekeza kuwepo na Bodi ya wana-IT ambayo itasimamia uvumbuzi wa teknolojia ndani ya nchi yetu kuliko kutumia wataalam kutoka mataifa ya nje kama ilivyo sasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, softwares & database; nashauri Serikali yetu ianze kutumia Open Source na STO Commercial Softwares ili kupunguza gharama za manunuzi na za uendeshaji. Kwa mfano, Postgress, SQL server, Geo- Network, Geo-Server, Survey Gizmo na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, TTCL, National Internet Data Centre. Pamoja na kujenga data centre naomba iwe very strong na ijengwe maeneo tofauti tofauti ili back-ups ziwe mbali na systems.