Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. JUMAA H. AWESO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nikushukuru kwa kunipa nafasi nami nichangie hotuba hii muhimu ambayo ni sekta yenye mchango mkubwa kwa maendeleo ya Taifa letu. Pili, nimpongeze Mheshimiwa Waziri na Naibu wake na watumishi wote wa Wizara hii. Binafsi nimevutiwa na utendaji wao wa kazi kama kauli ya Mheshimiwa Rais wetu ya Hapa Kazi tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze pia Mheshimiwa Rais kwa ahadi zake kwenye Jimbo la Pangani na kuzitekeleza kwa wakati kwa kutupatia kivuko kipya cha MV Tanga na kutupatia fedha za ujenzi wa geti, umetugawia na tumekabidhiwa mradi huu muhimu wa geti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie maeneo yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara; ujenzi wa barabara ni kichocheo cha shughuli za kiuchumi na hata kuongeza ajira. Maeneo ambayo yamebadilika kwa kiasi kikubwa katika uchumi hata huduma za kijamii yana barabara nzuri. Niombe Wizara hii iangalie kwa umuhimu wake Ujenzi wa barabara ya Tanga – Pangani – Saadani – Bagamoyo, ambayo ni ahadi ya muda mrefu. Hivyo ni wakati wa kujenga barabara hii ili iifanye Wilaya ya Pangani ipate maendeleo kutokana na fursa nyigine 21 zilizopo Pangani, ikiwemo Mbuga ya Wanyama ya Saadani. Pia ujenzi wa barabara hii uende sambamba na ulipaji wa hatua kwa hatua kwa wananchi wangu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Gati ya Pangani. Tunashukuru kwa kutujengea gati hili. Pia naomba Serikali ili gati hili liwe na tija na kuweza kupata mapato kuanzishwe usafiri wa majini, kwa maana ya kutupatia fast boat ya kutoka Pangani kwenda Mkokotoni. Mwekezaji ameshapatikana, cha muhimu ni kumpa ushirikiano wa dhati katika kufanikisha upatikanaji wa boat hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Mawasiliano; jamii ili ipige hatua ya maendeleo lazima iwe na mawasiliano ya uhakika, hii itachangia urahisishaji katika shughuli za kijamii na kiuchumi. Hivyo, Serikali itusaidie mawasiliano kwa maeneo ya Mkalamo, Mrozo na Bushori.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na naomba niunge mkono hoja kwa asilimia mia moja.