Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya kilometa 149 iliyomo kwenye Ilani ya CCM ya mwaka 2015 – 2020 inayoanzia Tabora – Mambali – Bukene – Kagongwa haimo kabisa katika kitabu cha Mheshimiwa Waziri cha bajeti ya 2017/2018.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii ilishindikana kufanyiwa upembuzi yakinifu mwaka wa jana kwa kuwa fedha iliyokuwepo kwa kazi hii milioni 400 haikutosha. Nilitarajia kuwa mwaka ujao wa fedha wa 2017/2018 barabara hii ingeongezewa fedha shilingi milioni 400 zingine ili zifike milioni 800 ambazo zingetosha kwa ajili ya kufanyia upembuzi yakinifu. Nimepitia kitabu chote na nimepitia miradi yote ya barabara kwa mwaka 2017/2018 lakini sijaona barabara hii ya Tabora – Mambali – Bukene – Kagogwa kilometa 149.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niliwasilisha jambo hili kwa Naibu Waziri Mheshimiwa Edwin Ngonyani ambaye aliongea na Meneja na TANROADS wa Tabora Ndugu Ndabalinze, lakini sijapata mrejesho wowote. Naomba barabara hii ipate fedha za kufanya upembuzi yakinifu ili tutimize ahadi ya CCM kama ilivyo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM.