Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Ujenzi wa Madaraja; nashauri Serikali na Wizara hii kuweka kipaumbele cha ujenzi wa madaraja yaliyo katika mipaka ya nchi hasa Malawi kwani hakuna madaraja yatakayoweza kusaidia tukipata dharura kama nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, usumbufu kwa magari katika mpaka. Kumekuwa na usumbufu wa foleni ndefu katika mipaka hasa magari makubwa ya usafirishaji ya transit.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vifaa vya Uokoaji. Kumekuwa na uhaba wa vifaa vya uokoaji majini hasa katika boti katika ziwa Tanganyika. Tunaomba Wizara ihakikishe inaweka vifaa hivyo kwani waathirika wakubwa ni wanawake na watoto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha ni kidogo katika Halmashauri ya Rungwe. Katika Wilaya ya Rungwe hakuna fedha za ujenzi/ukarabati wa barabara za ndani wakati Halmashauri hii ni muhimu kwa mazao ya chakula yanayozalishwa hapo.