Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Omar Abdallah Kigoda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. OMARI A. KIGODA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa napenda kumpongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu wake kwa jitihada wanazofanya katika kuimarisha miundombinu yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ya mikakati ya nchi ni kuhakikisha barabara za kufungua mikoa zinafanyiwa kazi kwa kujengwa kwa kiwango cha lami ili kuinua uchumi wetu katika Sekta ya Usafirishaji.

Mheshimiwa barabara ya Magole - Mziha - Handeni ni moja ya barabara zilizopo kwenye mpango huo. Licha ya kuwa kwenye mpango mkakati, pia ni barabara iliyopo kwenye Ilani ya Uchaguzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishukuru Wizara kwa kutengea fedha kipande kilichobaki ambacho ni kidogo sana. Mwaka 2016 katika bajeti tuliambiwa Mkandarasi anadai; naomba Mheshimiwa Waziri akija kujumuisha, atufafanulie ile shilingi milioni 100 iliyotengewa ile barabara ni ya matumizi gani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naomba kupata ufafanuzi, shilingi milioni 500 iliyotengewa barabara ya Handeni – Kiberashi – Kibaya – Singida ni kwa matumizi gani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, napenda kuunga mkono hoja.