Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii nami nichangie katika Wizara hii ambayo kwa hakika sasa inatenda haki na inafanya kazi ambazo zinaonekana kwa kila mtu ikiwemo katika Jimbo langu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kitabu cha hotuba ya Mheshimiwa Waziri ukurasa wa 164 wameonesha barabara hii ya Makongorosi hadi Mkiwa kipande cha Nolanga – Itigi – Mkiwa kilomita 56.9 zitajenga kwa kiwango cha lami. Shida kubwa iliyopo pale tayari ujenzi unakaribia kuanza, lakini mpaka sasa hivi hakuna ufidiaji kwa maana ya compensation kwa wale ambao wanafuatwa na barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri sasa azingatie kwamba wanapokwenda kujenga barabara, kuna wananchi wa Itigi ambao wamefuatwa na barabara hii ambayo ni kubwa inayojengwa mwaka huu, waweze kulipwa mapema kuondoa usumbufu ambao utajitokeza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niipongeze Wizara hii kwa kazi nyingi ilizofanya, lakini katika Jimbo langu kuna changamoto kidogo. Mheshimiwa Waziri, Profesa Mbarawa wakati anatembelea barabara hii kutoka Mbeya hadi Itigi alikutana na changamoto kubwa sana ya mawasiliano. Kuna shida, hakuna minara ya mawasiliano maeneo mengi, kwa hiyo nimwombe sana Mheshimiwa Waziri akumbuke maeneo yale aliyopita kutokea kule Rungwa, Mwamagembe, Kintanula na maeneo ya Vijiji vya Mkoa wa Tabora ambavyo katikati yake vinaingiliana na eneo hili hadi kufika Kalangali. Maeneo haya mwenyewe aliona mawasiliano ni shida. Kwa hiyo, nichukue nafasi hii kuwakumbusha waweze kuliona Jimbo la Manyoni Magharibi, kwa kweli mtandao wa barabara utasaidia lakini pia mawasiliano ni shida, hilo tu nilitaka kukumbusha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nipongeze pia Serikali yangu kwa kuamua kujenga reli ya kiwango cha standard gauge, pale walipoanzia lakini naomba sasa wafanye jitihada wasogee ifike hadi Itigi kwa kipindi kijacho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.
Ahsante sana.