Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. FREDY A. MWAKIBETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nipo. Kwanza nashukuru kwa kunipa nafasi hii ili niweze kuchangia Wizara hii muhimu. Nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri ambazo anazifanya katika nchi yetu ya Tanzania. Tumeshuhudia jinsi ambavyo anajenga flyovers, tumeshuhudia jinsi ambavyo nchi yetu imeingia mikataba ya kujenga standard gauge katika reli ya kati, tumeshuhudia jinsi ambavyo majengo ya hosteli Dar es Salaam yamekamilika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Wizara hii kwa upande wetu wa Busokelo kuna barabara ambayo inaanzia Katumba – Luangwa - Mbambo mpaka Tukuyu, ina urefu wa kilometa 83. Hata kwa haya ambayo tumepata si haba, tunakushukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa jinsi ambavyo umeshiriki kikamilifu pamoja na wataalam wako. Bado tunaomba kwa kuwa kilometa ambazo umetupa sasa hivi bado hazijatosheleza zile kilometa 83. Kwa hiyo, tunaomba ikiwezekana katika bajeti yako uweze kutuongezea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona pia jinsi ambavyo Wizara inavyofanya kazi vizuri hasa katika suala la mawasiliano. Nitoe ushauri wangu katika mambo machache hasa TCRA. Tumeaona jinsi watu wengi sana tunatumia mifumo hii ya simu lakini kwa bahati mbaya inatumika hata kwa njia ya uhalifu na TCRA wanashindwa kudhibiti na hata wakati mwingine watu wanatuma meseji za kutukana wenzao, kwa hiyo tulitaka mifumo hii iboreshwe vizuri ili wawe na mfumo ambao unaweza uka-filter, maana kila utakapokwenda TCRA wanakwambia hatujui ama mfuate mwenye namba fulani. Kama kutakuwa na systems ambazo zinaweza zikafanya kazi vizuri, bila shaka uhalifu ambao unaendelea sasa hivi nchini kwa kutumia njia ya mtandao hautakuwepo tena. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nichangie katika suala la mifumo ya kompyuta, ukisoma kitabu cha Waziri ukurasa wa 202, wamesema watajenga National Internet Data Center. Napenda nishauri kama Mtaalam wa Mifumo ya Kompyuta, unapojenga Data Center ya nchi ambapo mtakuwa mna-share information mbalimbali, haitakiwi iwe centralized sehemu moja, iwe decentralizide ili ikitokea in case kuna any emergencies zile backups ziweze kufanya kazi vizuri, kama nchi za wenzetu za Ulaya wanavyofanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nashauri katika jambo hili la mawasiliano, mara nyingi sana katika nchi yetu tunatumia soft ambazo tunasema ni commercial, commercial kwa maana ya kununua hizo software, lakini kama tungekuwa tunatumia software ambazo ni open source na gharama yake ni ndogo ni rahisi kuzi –maintain kwa maana ya sustainability yake inakuwa ni kubwa kuliko hizi commercial software ambazo tunanunua kwa gharama kubwa na kuzi-maintain kwake ni gharama kubwa vilevile. (Makofi)

Kwa hiyo, ningeshauri Serikali ianze sasa kama Mataifa mengine ambayo yameanza hasa nchi za Ulaya Magharibi zinafanya hivyo, lakini ukienda Marekani wanatumia zaidi hizi microsoft ambazo ni gharama kuzi-maintain lakini pia kuna software nyingi ambazo ningeweza pengine kuzitaja kuna hizi Postgrace, Oracle, Square Server, Survey, GSMO, kwa sababu nimeishi nazo naweza nikaishauri Serikali iweze kufanya hivyo. Pia kuna software nyingi, kuna nyingine ambazo zinatumika kwa ajili ya kuisaidia nchi iweze kupata mapato yake vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wewe ni shahidi sasa hivi Serikali ikitaka kupata mapato mazuri kutoka kwenye mitandao ya simu lazima waende kwenye mobile operator mwenyewe kwamba sasa mwezi huu umepata kiwango gani, wakati ilitakiwa wawe na mfumo ambao wao wanapeleka direct. Kwa hiyo, kila muamala unaofanyika either uwe wa pesa ama uwe wa simu Serikali iwe inajua kwa kiwango gani inaweza kupata mapato yake kupitia kwenye mifumo hii ya simu. Kwa sasa hivi Serikali inaibiwa sana kwa sababu hatuna hiyo mifumo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi za wenzetu ambazo zimeendelea sasa ukienda kama Ethiopia, Afrika Kusini na nchi nyingine za Ulaya wana mifumo ambayo inakuwa centralized siyo kama sasa hivi ambavyo imekuwa decentralized. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niweze kumalizia kwa upande wa TBA. TBA inafanya kazi nzuri na nimeambiwa pia kwamba mmepewa kazi ya kujenga majengo ya Halmashauri mbalimbali nchini. Kwa bahati mbaya sana TBA katika baadhi mikoa hampo ikiwemo hata kule kwetu katika Jimbo la Busokelo, katika mkoa mzima wapo watatu tu. Kwa hiyo, fedha za Halmashauri nyingi mpya ambazo zimepewa zipo tu kwenye akaunti za Halmashauri na karibu mwaka wa fedha unakwisha. Tunapofuatilia na kufuatilia wanakwambia wamepewa kazi TBA. Kwa hiyo, tunaomba kama TBA watajenga na kwa kweli wanajenga kwa kiwango kizuri na kwa gharama nafuu, basi iongezewe uwezo zaidi ili iende hadi huko mikoani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, napenda kuunga mkono hoja. Ahsante sana.