Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Selemani Said Bungara

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. SELEMANI S. BUNGARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kukuwezesha wewe kuwa Mwenyekiti wa kikao hiki na namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kumpa Urais Mheshimiwa Magufuli na kuapa kwamba atailinda Katiba ya Jamhuri ya Tanzania, lakini kwa bahati mbaya tu Katiba yenyewe kidogo anaipindisha pindisha kwa sababu hatoi haki kwa Vyama vya Siasa kufanya mikutano. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, si nimetoa shukrani? Mimi nimetoa shukrani tu wala sikumtukana mtu yeyote. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kutoa shukrani hizi kwa Mwenyezi Mungu leo najielekeza kuchangia katika sehemu mbili tu katika hotuba hii. Tunakumbuka 2010 Rais aliyemaliza muda wake Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete Mungu amzidishie, aliahidi kwamba katika kampeni yake ya 2010 aliahidi kwamba atatengeneza barabara ya Kwa Mkocho – Kivinje barabara ya kilomita 4.2 kwa kiwango cha lami, mpaka leo nisemavyo barabara kwa mvua za jana tu na juzi gari zilikuwa hazifiki katika Hospitali ya Wilaya kutokana na barabara hiyo kuwa chafu na haipitiki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Bajeti ya 2016/2017, tulitenga milioni 800 kwa ajili ya barabara hiyo ili ikamilike kwa kiwango cha lami, lakini mpaka sasa hivi nisemavyo ndege zimenunuliwa lakini fedha hizo za bajeti hazijaingia katika Wilaya ya Kilwa ili barabara hiyo itengenezwe. Pamoja na ndege mlizonunua hizo lakini mkumbuke kwamba kuna barabara ambazo ni muhimu sana zinaenda katika hospitali za Wilaya, nazo zikumbukwe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri naomba hizo milioni 800 zipatikane ili babaraba ile iishe. Tena kwa bahati nzuri tarehe 2 Machi, 2016 Rais wa Jamhuri ya Muungano Mheshimiwa Dkt. Magufuli alifika Kilwa na nikamwambia tatizo hilo kwamba kuna kiporo cha Rais aliyepita na nikamwomba kiporo hicho amalizie yeye. Akaahidi na kumuagiza Injinia kwamba hiyo barabara iishe.

Naomba sana naomba, kwa kuwa Mheshimiwa Magufuli hasemi uwongo na alisema kwamba barabara lazima naomba barabara hiyo iishe ili watu wapate kutumia barabara hiyo na kufika katika hospitali kwa njia ya usalama. Bila hivyo watu wa Kivinje na Wilaya ya Kilwa kwa ujumla tutaona kwamba hatutendewi haki tunaonewa bila sababu ya msingi. Naomba Mheshimiwa Waziri barabara hiyo iishe na fedha hizo milioni 800 zipatikane katika mizezi mitatu iliyobaki ili barabara hii iishe. Hilo la kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili ni uwanja wa ndege. Kilwa Masoko kuna uwanja wa ndege, uwanja huo kulifanywa tathmini kwa wananchi wangu tarehe 19 Machi, 2013 ili walipwe fidia ili uwanja upanuliwe. Mpaka leo ninavyoongea tangu 2013 mpaka leo 2017 wananchi wangu hawajapata fidia. Naomba sana katika kuhitisha hotuba yake Mheshimiwa Waziri atuambie hawa wananchi wangu watapata lini fidia hiyo ya uwanja wa ndege na kama haiwezekani mseme kwamba haiwezekani.
heshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, ingawa dakika tano hazijatimia lakini imeeleweka.