Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Dr. Joseph Kizito Mhagama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Madaba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze kwa kukushukuru wewe kwa kunipa hii nafasi na nimshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kupata nafasi ya kuchangia katika Wizara hii muhimu sana ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.
Mheshimiwa Naibu Spika, nitachangia katika maeneo makubwa mawili na iwapo muda utaniruhusu, nitaongeza sehemu ya tatu. Kwanza kabisa, niungane na Waheshimiwa Wabunge wote ambao wamempongeza sana Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri anayoifanya kwa kupitia Wizara hii ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. Nisingependa kurudia maneno mazuri ambayo Wabunge wengi wamesema kuhusu kazi nzuri zilizofanyika, Tanzania sasa imeunganishwa kwa barabara nyingi, inaunganishwa kwa reli, lakini inaunganishwa kwa anga. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nachukua nafasi hii kutambua mchango mkubwa sana wa Mawaziri kwa kumsaidia Mheshimiwa Rais na kesho sisi wadau wa Mkoa wa Ruvuma tutakuwa pale Songea tarehe 30 kupokea ndege aina ya Bombardier ikitua kwa mara ya kwanza katika Mji wa Songea. Kwa hiyo, ni kazi nzuri ya Wizara hii, nachukua nafasi hii kuipongeza sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, yapo maeneo matatu ambayo napenda niishauri Wizara au Serikali katika ujumla wake. Eneo la kwanza, hii miradi tunayowekeza ni mikubwa sana. Wizara ya Nishati inawekeza katika miradi mikubwa sana na Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano nao wanawekeza katika miradi mikubwa sana. Wizara hizi mbili, ili miradi hii inayowekezwa iweze kuwa na tija, ni muhimu sana hizi Wizara mbili zikafanya kazi kwa ukaribu sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, unajua sisi Jimbo la Madaba tunapakana na eneo lenye mradi mkubwa sana, tunaita Flagship Projects pale Liganga na Mchuchuma. Huu ni mradi mkubwa sana na ni mradi ambao umezungumziwa kwanza kabisa na Mheshimiwa Profesa Simon Mbilinyi, baadaye akafuatia Mheshimiwa Waziri Jenister Mhagama. Mimi leo ni Mbunge wa tatu katika Bunge lako kuzungumzia mradi huu kutoka eneo hilo hilo la Jimbo.
Mheshimiwa Naibu Spika, mradi huu umechukua muda mrefu sana, lakini sasa mradi huu una matumaini makubwa ya kuanza; na taratibu zote za kuanza zimekamilika na tutaisikia kwenye Wizara wa Nishati na Madini watakapowakilisha. Kinachosikitisha ni kwamba hakuna maandalizi ya kutosha kuhakikisha kwamba barabara zinazokwenda kwenye mradi huu mkubwa zinakamilika. Huwezi kuzungumzia Mradi wa Lingaganga na Mchuchuma bila kuzungumzia barabara inayotoka Madaba kwenda Mkiyu - Linganga. Utawezaje kusafirisha mitambo kwenda katika eneo la mradi? Utawezaje kuvuna makaa na chuma kutoka katika eneo la mradi? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, yawezekana Wizara kwa sababu moja au nyingine na yawezekana ni sababu za msingi kwamba hawajaweka bajeti ya kutosha ya kukamilisha barabara hii kwa kiwango cha lami, nawaomba Wizara, kama kweli tupo serious na kama kweli Miradi ya Mchuchuma na Linganga inaanza, lazima barabara ya Madaba - Mkiyu ikamilike. La sivyo, tutaiingiza Serikali kwenye hasara kubwa sana. Mradi upo tayari kuanza lakini barabara ya kwenda kwenye mradi haipo. Hatuwezi kufanikiwa tusipoweza kuunganisha haya mambo.
Mheshimiwa Naibu Spika, eneo la pili linahusu Mfuko wa Barabara Vijijini. TAMISEMI wanapata asilimia 30 ya fedha zote zinazokusanywa kwa ajili ya Mfuko wa Barabara na asilimia 60 inabaki kwa TANROADs kwa ajili ya kushughulikia barabara za mikoa na hii asilimia 30 inakwenda TAMISEMI na inakuwa translated kwenye kutekeleza miradi ya barabara ndani ya Halmashauri. TAMISEMI wanakuja na wazo kwamba tuwe na Rural Road Agency, hili wazo ukiliangalia kwa haraka, linaonekana kama ni zuri na lenye tija, lakini niliomba ni-draw attention ya TAMISEMI na Wizara ya Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano. Kwanza lazima tujue kwamba kama kumekuwa na ufanisi katika ngazi za Halmashauri zetu, ni kwa sababu wale wanaofanya kazi katika Halmashauri za Wilaya wapo accountable moja kwa moja kwa wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hiyo sense of accountability ndiyo inayofanya Halmashauri zetu ziwe na tija (efficiency) kwa sababu anayesimamia miradi katika Halmashauri ni Diwani ambaye yupo karibu na wananchi, anajua matatizo ya wananchi na anawajibika kwa wananchi. So sense of accountability imeleta tija sana katika utekelezaji wa miradi katika ngazi ya Halmashauri.
Mheshimiwa Naibu Spika, ukilinganisha na taasisi au agency mbalimbali zinazoundwa zenye hadhi ya Kitaifa sense of accountability haiwezi kuwa sawa. Halmashauri sense ya accountability ni kubwa zaidi. Naomba sana, tusi-attempt kutengeza huu Mfuko wa Barabara Vijijini, isipokuwa fedha hizi zigawanywe kwa uwiano sawa katika Halmashauri na ziendelee kusimamiwa na Halmashauri za Wilaya zetu. Italeta tija zaidi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kingine najua TANROADs hakuna urasimu sana, lakini taasisi yoyote yenye muundo ina urasimu. Halmashauri zina urasimu, TANROADs wana urasimu na Taasisi yoyote ina urasimu kwa sababu ya muundo wake. Sasa ukilinganisha level ya urasimu katika Taasisi za Kitaifa na Halmashauri, Halmashauri level ya urasimu ipo chini sana. Kwa hiyo, tutumie hiyo fursa sasa kupeleka hizi fedha zikafanye kazi kwa tija katika Halmashauri, tukiziacha kwenye ngazi hizo za juu hatutapata ufanisi. (Makofi)
Mheshimwa Naibu Spika, pia ningeweza kusema, kwangu mimi kufikiria kutengeneza hii tunayoita Mfuko wa Barabara Vijijini kwa maana ya Rural Road Agency, katika context ile ile na mfananisho ule ule wa TANROADs ni jaribio la kudhoofisha dhana ya ugatuzi wa madaraka. Kwa hiyo, naiomba sana Serikali ifanye study upya ya efficiency za Halmashauri zetu ukilinganisha na efficiency ya agency mbalimbali zenye hadhi ya Kitaifa ili kuleta tija.
Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho kama muda unaniruhusu, nichangie tu kwamba ukisoma katika hiki kitabu unaona kumekuwa na shida kidogo katika allocations za projects. Ipo mikoa ambayo imepata miradi mingi zaidi kuliko mingine. Sababu zinaweza zikawa za msingi kwa maana ya mahitaji halisi, lakini ni vizuri sasa niiombe Serikali iangalie priorities nyingine pia.
Mheshimiwa Naibu Spika, leo tumewekeza fedha nyingi sana kujenga Jiji la Dar es Salaam ambalo lina wananchi milioni tatu na zaidi kidogo…
Wanakaribia milioni tano, lakini tukumbuke pia mahitaji katika maeneo mengine ni muhimu pia. Naiomba Serikali sasa iangalie, ifanye rationalization ya miradi yake. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa vile muda hauniruhusu, nakushukuru sana na naunga mkono hoja.