Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi kuchangia mada iliyopo mezani. Kwanza namshukuru Mungu kwa kuwa na afya njema. Napenda kuchangia kwa ujumla na sehemu nyingine kutoa ushauri kwa Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza napenda kuchangia juu ya ucheleweshaji wa pesa kutoka Serikalini kwenda kwenye Wizara na madhara yanayopatikana kwa ucheleweshaji huo.
Mheshimiwa Naibu Spika, wakati tunatembelea miradi, tumekuta kwamba kutokana na ucheleweshaji wa fedha hizo, madhara yaliyojitokeza ni gharama za ujenzi kuongezeka mara mbili. Mfano, barabara iliyojengwa kutoka Dumila kuelekea Ludewa, badala ya kujengwa kwa shilingi bilioni 42 imejengwa kwa shilingi bilioni 42 plus variation ya shilingi bilioni 22. Unaangalia, unasikitika na kukuta kwamba hali hii itasababisha ujenzi wa kilometa chache mahali ambapo ingeweza kujengwa kilometa nyingi kutokana na hizo variations.
Mheshimiwa Naibu Spika, ukumbuke kwamba kunapotokea variations kubwa kama hizo, kuna negotiation, ndipo loophole zile za ufisadi zinapoingia. Kwa hiyo, naishauri Serikali kama ina nia ya dhati ya kuhakikisha kilometa nyingi
zinajengwa kama walivyojipangia, wapeleke fedha kwa wakati ili kutokuruhusu hizo variations ambazo zina mianya ya ufisadi.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuchangia kwenye viwanja vya ndege. Kwenye viwanja wa ndege tumetembelea; nimekuta kwamba vingi viko chini ya viwango, kiasi kwamba pamoja na ununuaji wa ndege zilizonunuliwa, lakini viwanja vya ndege bado vingi ni vibovu. viwanja vya Shinyanga, viwanja vya Moshi. Moshi, kiwanja ambacho kina mlima wa Kilimanjaro ambapo ungeweza kuleta mapato makubwa, unavitegemea viwanja vitatu ambavyo vinazalisha. Sasa ukiwa na viwanja ambao vinazalisha na viwanja vinavyo-consume, ujue bado hujafanya kazi ya faida.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naishauri Serikali, kama ina nia ya dhati ya kutengeneza pato kwa Taifa, ihakikishe kabisa viwanja hivi vinavyo-consume faida inayotoka kwenye viwanja vile vinavyozalisha, inavitengeneza na viweze kufanya kazi na viweze kuleta faida. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pia napenda kuchangia sehemu ya bandari. Bandari yetu ya Tanzania tofauti yake na bandari nyingine za wenzetu ni kwamba bandari ya Tanzania kwa mfano, kwenye ushushaji wa mafuta.
Mheshimiwa Naibu Spika, nchi za wenzetu mafuta yanashushwa kwenye matenki ya Taifa na flow meter inakuwepo tanki la Taifa, ndilo linalogawanya mafuta yale kwenye matenki ya watu binafsi. Sisi kama Tanzania unakuta kwamba matenki ni ya watu binafsi. Kwa hiyo, sisi tunahangaika na flow meter kugawanyia kwenye matenki ambayo siyo ya kwetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri Serikali ijitahidi kuhakikisha kwamba manteki ya Taifa yanakuwepo ili tunapopata mafuta tuweze kugawa kwenye mantaki ya wafanyabiashara ili Taifa liweze kupata faida.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda nichangie miundombinu na mwanamke. Napenda hii lugha kwa sababu nafahamu kabisa mwanamke wa Tanzania ndiye anayezaa watu wote tulioko hapa; ametuzaa mwanamke, lakini hakuna hata mtu mmoja hajui kama huyu mwanamke alizalia wapi, alisafiri kwa usafiri gani mpaka akafika sehemu aliyojifungulia. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tukiliangalia hilo kwa jicho la uchungu, tutafikiria barabara za vijijini ziboreshwe, mgao ule inaogawa Serikali ihakikishe kwamba inagawa mgao ambao utasababisha barabara za vijijini kujengwa kwa viwango ambavyo mama mjamzito akiwa anaenda kujifungua, hataweza kufia njiani. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nina mfano hai kabisa, nina ndugu yangu ambaye alibebwa kwa toroli, akawa anatembezwa kupelekwa hospitali. Zile kukuru kakara zote, akapata rupture njiani na akafia njiani. Yote hiyo ni kwa sababu tu barabara zile zilikuwa ni mbovu na hakuna njia nyingine, ilikuwa ni kumbeba aidha kwa mzega ama kwa toroli. Sasa tufikirie kama Serikali, huyu mwanamke ambaye ndiye anayezalisha mashambani huko, akitaka kupeleka mazao sokoni anashindwa apitishe wapi ili akafikishe sokoni? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mwanamke huyo ndiye ambaye anazaa; anapohitaji kujifungua, hajui apite njia gani mpaka afike hospitali, ukuzingatia kwamba Tanzania sasa hivi bado hatujafika sehemu kila kijiji kuwa na hospitali.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Serikali iliangalie hilo na ichukue umuhimu kuhakikisha kwamba mafungu yale yanawafikia na uwezekano wa kupata barabara ambazo zinapitika ili kurahisisha hawa wanawake waweze kujifungua vizuri na uzazi salama uweze kupatikana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuchangia eneo la DARTS. Nimeangalia Dar es Salaam mradi wa DARTS, ni mpango mzuri kabisa. Pia kuna treni ile (commuter), naomba basi, kwa sababu tulitembelea na nikaona jinsi gani kama ile commuter itapata vichwa ambavyo siyo long safari, inaweza kuleta faida kubwa kabisa, tena faida ya wazi kabisa.
Mheshimiwa Naibu Spika, tulifanya calculations tukakuta kwamba kwa kupata short safari, vichwa na mabehewa yake tunaweza tukatengeneza faida na Wizara hii ikaweza kuleta faida kubwa kuliko inavyotegemea. Kwa sababu sasa hivi treni ile ya pale Dar es Salaam inayoenda Pugu inatumia vichwa vya long safari, kwa hiyo, mafuta yanayotumika ni mengi. Kwa hiyo, inashindwa kuleta faida tarajiwa. Natamani kuona ile treni inapata vichwa na mabehewa ya short safari ili iweze kutengeneza faida iliyotarajiwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nichangie upande wa TCRA; napenda kupongeza TCRA kwa kazi nzuri wanayofanya ambayo ina faida kubwa, lakini pia naomba Serikali iangalie TCRA kwa macho ya huruma kwa sababu maduhuli inayokusanya inapeleka Serikalini hela nyingi, lakini mrejesho wake unakuwa ni wa shida sana kwa ajili ya urasimu wa kurejesha zile hela ili TCRA waweze kufanikisha utendaji wao. Hivyo naishauri Serikali kwamba kwa kuwa TRCA wanafanya kazi nzuri, basi ni vizuri wanapoomba pesa ili waweze kuleta utendaji mzuri, waweze kurejeshewa kwa wakati.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia naomba kuchangia kuhusu Data Center ya Taifa ambayo iko chini ya Wizara hii. Naishauri Serikali kuhakikisha kwamba taasisi zote za Serikali zinatumia Data Center ile iweze kufanya kazi iliyotarajiwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kusema hayo, nashukuru sana.