Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. VEDASTUS M. MANYINYI: Mheshimiwa
Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri nakupongeza kwa hotuba yako nzuri, nami naunga mkono hoja. Pamoja na pongezi hizo napenda kupata ufafanuzi mdogo, mwaka jana Jaji Mkuu alipokwenda Musoma pamoja na shida mbalimbali na hoja zilizotolewa mbele ya Jaji, moja ilikuwa posho za Wazee wa Baraza kulipwa 5,000/= kwa kesi, vilevile kucheleweshwa malipo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jaji Mkuu aliwaahidi wale Wazee wa Baraza kulipwa 10,000/= badala ya 5,000/=. Mpaka sasa wale Wazee wa Baraza wanalipwa 5,000/= na cha ajabu toka mwaka jana mwezi Septemba hawajalipwa hadi leo. Mheshimiwa Waziri, ikumbukwe kwamba, wazee hawa wanakwenda Mahakamani tangu asubuhi hadi mchana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba ufafanuzi na majibu ya maslahi ya wazee hawa. Ahsante na naomba kuwasilisha.