Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naanza kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa hotuba yake nzuri na pili, naunga mkono hoja. Napenda kujielekeza katika ujenzi wa Mahakama ya Mwanzo hasa katika halmashauri mpya kama ilivyo Halmashauri yangu ya Itigi. Pia, kuna upungufu mkubwa wa Mahakimu wa Mahakama za Mwanzo na hata watumishi katika mahakama hizi. Nashauri Wizara yake iajiri Mahakimu wa Mahakama za Mwanzo na hasa vijijini, kama ilivyo Jimbo langu la Manyoni Magharibi. Halmashauri za Wilaya zina hadhi sawa na wilaya ya kiserikali, hivyo zipewe hadhi ya kuwa na Mahakama za Wilaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri alitazame Jimbo langu la Manyoni Magharibi kwa jicho la kipekee katika ujenzi wa Mahakama za Mwanzo kwani, zilizopo ni chakavu na hazina hadhi, kama ilivyo Wizara yako ilivyo na heshima kubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha na narudia tena naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.