Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Joseph Leonard Haule

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mikumi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana nami niweze kuchangia kidogo kwenye Wizara hii nyeti ya Sheria na Katiba. Kumekuwa na malalamiko na kilio cha muda mrefu sana cha wafanyakazi walioachishwa kazi Kilombero Sugar Company mwaka 2,000. Wafanyakazi hao karibu 3,000 walipoachishwa kazi hawakulipwa stahiki zao na wamekuwa wakidai stahiki zao hizo kwa muda mrefu sana, wengine wameshatangulia mbele za haki na wengine bado wapo hai. Wafanyakazi hao walipoona hawatendewi haki walikwenda Mahakamani na kukawa na Jalada la Kesi Namba 50/2000.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wafanyakazi hao wamekwenda mara kadhaa Wizara ya Katiba na Sheria wakiomba wapewe nakala ya hukumu ya jalada lao la kesi Namba 50/2000 bila mafanikio. Pia, waliandika barua kwa Waziri wa Wizara ya Katiba na Sheria tarehe 24 Machi, 2016 na nakala kupelekwa kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu ambaye mnamo tarehe 25 Julai, 2016 (Kumb. Na. PM/P/1/569/82), Katibu wa Waziri Mkuu alijibu kuwa ameipata na ataisisitiza Wizara ya Katiba na Sheria ishughulikie kikamilifu kwa mujibu wa Sheria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mnamo mwaka 2014 Mahakama Kuu iliwapatia tamko la kuvumilia na kwamba, walikuwa wakilifanyia kazi, mpaka sasa hakuna majibu. Ndipo walipoamua kulipeleka Wizara ya Katiba na Sheria mwezi Julai, 2016.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo, kwa niaba ya wafanyakazi walioachishwa kazi Kilombero Sugar Company 2000, namwomba Waziri atakapokuja kwenye majumuisho yake aje atupe majibu kwamba, ni lini sasa wananchi hao watapata haki yao ya kupata nakala ya hukumu ya kesi Namba 50/2000. Ni matumaini yangu mtawasaidia kilio cha wanyonge hawa, ili wapate haki yao ya kulipwa mafao yao wanayostahili ambayo wamekuwa wakiyapigania kwa muda mrefu sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.